Thursday, November 30, 2017

Naibu Waziri afanya Mazungumzo na Balozi wa Saudi Arabia nchini

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Suzan Kolimba(Mb) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Saudi Arabia nchini Mhe. Balozi Mohammed M. Almalik alipomtembelea wizarani tarehe 30/11/2017. Lengo la Mazungumzo hayo ni kuzungumzia mahusiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia, Mhe.Balozi alisema hadi sasa Saudi Arabia wana jumla ya miradi  6 katika eneo la maji na afya, kati ya hiyo 3 iko Tanzania bara na 3 Zanzibar.

 
Mhe. Naibu Waziri Dkt Kolimba na Mhe. Balozi Almalik wakiendelea na mazungumzo, wanaofuatilia mazungumzo hayo ni Bw. Charles Faini Msaidizi wa Naibu Waziri(kulia) na anayefuata ni Bw. Odilo Fidelis, Afisa Mambo ya Nje.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.