Friday, April 28, 2023

NJE SPORTS CHUPUCHUPU KUTWAA UBINGWA WA KARATA

Timu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports) iliyopo jijini Morogoro kushiriki katika michezo mbalimbali inayoendelea mjini hapo kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Mei Mosi imejitosa kuwania ushindi katika mchezo wa karata na drafti. 

Katika michezo hiyo iliyochezwa kwa nyakati tofauti ilianza na hatua ya makudi na kufuatiwa na robo fainali, nusu fainali, na fainali. 

Kwa upande wa mchezo wa karata Nje Sports iliwakilishwa na Bw. Peter Ndatila na Bi. Nyanzala Lupeja. Bi. Lupeja ambaye aliwakilisha upande wa Wanawake - Nje Sports alifanikiwa kufika hatua fainali na kuibuka mshindi wa 4 baada ya kuonesha umahiri wa hali ya juu uliomfanya kuvuka hatua ya makundi, robo na nusu fainali. Bi. Lupenja kupitia kundi B2 alifanikiwa kufuzu baada kujikusanyia alama 6 katika michezo 6 aliyocheza. 

Wakati huo huo ushindani mkali hulioshuhudiwa kwa upande wa Wanaume katika mchezo huo, ulitosha kufifisha juhudi na makali ya Bw. Ndatila na kumfanya ashindwe kufuzu katika hatua ya makundi. Bw. Ndatila alifanikiwa kujikusanyia alama 5 katika kundi D baada ya kusuluhu katika michezo yote 5 aliyocheza. Wachezaji wawili waliofanikiwa kufuzu kwenda robo fainali katika kundi hilo walijikusanyia alama 8 na 7 katika michezo 5 iliyochezwa.

Kwa upande wa mchezo wa drafti Nje Sports iliwakilishwa na Bw. Shaban Maganga ambaye licha ya kuonesha makali yake na kutoa upinzani mkali katika mchezo huo hakufanikiwa kuvuka kwenda hatua ya makundi. Bw. Maganga alijikusanyia alama 6 katika kundi E na kushika nafasi ya 4 kati ya washiriki 7 wa kundi hilo. Wachezaji wawili waliofanikiwa kupita kwenda robo fainali katika kundi hilo walijikusanyia alama 11 na 10 katika michezo 6 iliyochezwa.

Mashindano hayo ya michezo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Mei Mosi yanatarajiwa kuhitimishwa katika siku hizi mbili za mwishoni mwa Juma (Ijumaa na Jumamosi) mjini Morogoro, ambapo watumishi, wakazi wa Morogoro na maeneo jirani watapata fursa ya kutazama fainali katika michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, riadha na kuvuta kamba. 
Usajili wa washiriki wa mchezo wa drafti ukiendelea kwenye mashindano ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Mei Mosi uliofanyika kwenye uwanya wa Jamhuri mjini Morogoro
Mchezaji wa drafti wa Nje Sports Bw. Shaaban Maganga akijisajili kushiriki mchezo uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro
Mchezaji wa karata wa Nje Sports Bw. Shaaban Maganga (kushoto) akimkabili mpinzani wake katika mchezo wa karata uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro
Mchezo ukiendelea
Mchezaji wa karata wa Nje Sports Bi. Nyanzala Lupeja (kulia) akimkabili mpinzani wake katika mchezo wa karata uliofanyika Jamhuri mjini Morogoro
Mchezaji wa karata wa Nje Sports Bi. Nyanzala Lupeja (kushoto) akimkabili mpinzani wake katika mchezo wa karata uliofanyika Jamhuri mjini Morogoro
Mchezaji wa karata wa Nje Sports Bw. Peter Ndatila akimkabili mpinzani wake katika mchezo wa karata uliofanyika Jamhuri mjini Morogoro
Mchezo ukiendelea
Mchezo ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.