Thursday, April 6, 2023

SERIKALI YAIHAKIKISHIA JUMUIYA YA KIMATAIFA IMEDHIBITI UGONJWA WA MARBURG

Serikali kupitia Wizara za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Afya imekutana na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi na taasisi zao hapa nchini  na kuwatoa hofu juu ya ugonjwa wa Mabarg ambao tayari umedhibitiwa.

Akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua za kukabiliana na kudhibiti ugonjwa wa marbug tangu ulipoanza na hadi sasa hakuna maambukizi mapya.

“Napenda kuwatoa hofu Mabalozi pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa kuwa Tanzania ni salama na hivyo tuendelee kufanya kazi zetu kama kawaida kwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya,” alisema Dkt. Tax 

Akizungumza kwa Niaba ya Waziri wa Afya, Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Tumaini Nagu amesema tangu ugonjwa huo ulipoibuka Serikali imechukua hatua za haraka za kudhibiti ugonjwa huo na hadi sasa hakuna maambukizi tena.

“Jumla ya visa vya ugonjwa huo vimebaki 8 na kati yao watu 5 wamefariki ,watatu wanaendelea na matibabu na mgonjwa mmoja ameruhusiwa na wagonjwa waliolazwa wanaendelea vizuri,” alisema Prof. Nagu

Kwa Upande wake Kiongozi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comorro nchini, Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed ameipongeza Serikali kwa hatua ilizochukua za kutoa taarifa za ugonjwa wa Maburg kwa wakati.

“Tunaipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua ilizochukua kuukabili ugonjwa wa Maburg ikiwemo utoaji sahihi wa taarifa, elimu kwa umma kuhusu ugonjwa huo,” alisema Dkt. El Badaoui Mohamed.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa (hawapo pichani) Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa Jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Kiongozi wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comorro nchini, Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed (kushoto) na Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Tumaini Nagu (kulia)

Balozi wa Marekani Nchini, Mhe. Michael Battle akichangia jambo wakati wa mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Rwanda Nchini, Mhe. Maj. Gen. Charles Karamba akichangia jambo wakati wa mkutano 

Balozi wa Rwanda Nchini, Mhe. Regina Hess akichangia jambo wakati wa mkutano 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akieleza jambo kwa Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wakati wa mkutano















No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.