Sunday, June 16, 2024
DKT. MPANGO AMWAKILISHA RAIS SAMIA KWENYE MAZISHI YA KITAIFA YA MAKAMU WA RAIS WA MALAWI
Saturday, June 15, 2024
NAIBU KATIBU MKUU MAMBIO YA NJE ATOA SALAMU ZA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU DKT. SHOGO
![]() |
Balozi Mussa na Mhe. Kawawa wakimfariji Prof. Eliamani Sedoyoka ambaye ni mume wa aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Marehemu Dkt. Shogo Mlozi. |
![]() |
Balozi Mussa na Mhe. Kawawa wakitoa faraja kwa wazazi wa marehemu. |
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imefanya ziara jijini Arusha leo tarehe 15 Juni, 2024 ili kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu.
Baada ya kuwasili Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Vita Kawawa aliyeambatana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa walipokelewa na Makamu wa Rais wa Mahakama hiyo, Mhe. Jaji Modibo Sacko.
Kufuatia umuhimu wa ziara hiyo kamati ilianza ziara kwa kufanya kikao na menejimenti ya Mahakama kilichoongozwa na Mhe. Jaji Sacko akiwa na mwenyekiti mwenza Mhe. Vita Kawawa.
Akiongea katika kikao hicho Mhe. Jaji Modibo Sacko ameishukuru Kamati ya Bunge kwa kuendelea kuipigania Bungeni Mahakama hiyo hususan katika kupata fedha za Maendeleo zinazowezesha kuendelea kwa ujenzi na kuwa na mazingira mazuri ya kufanyia kazi.
Naye Naibu Katibu Mkuu Mambo ya Nje, Balozi Mussa ameipongeza Mahakama kwa kuendelea kutekeleza majukumu yake ya kusimamia Haki za Watu kila inapotakiwa kufanya hivyo kulingana na itifaki ya uanzishwaji wake.
"Kamati imefanya ziara ili kujionea hatua iliyofikiwa katika ujenzi na pia tunashukuru kwa kuwa na kamati imara katika usimamizi wa majukumu hivyo, niwaondoe hofu kuwa Wizara itaendelea kusimamia ujenzi unaoendelea pamoja na kuzingatia thamani ya fedha," alisema Balozi Mussa .
Akiwasilisha salamu za shukrani Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Kawawa ameeleza kuwa Kamati yake inatambua umuhimu na majukumu makubwa yanayolotekelezwa na Mahakama hiyo katika kuimarisha haki barani Afrika, hivyo Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.
Mara ya mwisho Kamati ya Mambo ya Nje, ulinzi na Usalama kutembelea ujenzi wa mradi wa Mahakama hiyo ilikuwa mwezi Machi, 2023. Hata hivyo, wabunge hao kwa umoja wao wametoa pongezi kwa hatua nzuri ya ujenzi iliyofikiwa na kusisitiza usimamizi makini.
Mradi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ulianza ujenzi mwezi Agosti, 2023 na unatarajiwa kumalizika mwezi Februari, 2025 na utagharimu takriban shilingi za Kitanzania Millioni 22.97.
======================================
![]() |
Makamu wa Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, Mhe. Jaji Modibo Sacko akiishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ilipofanya ziara katika Mahakama hiyo jijini Arusha tarehe 15 Juni, 2024. |
![]() |
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu na Utawala katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi John Kiswaga akiwasilisha taarifa ya hali ya utekekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Mahakama katika kikao hicho. |
![]() |
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakipata ufafanuzi kutoka kwa msiamamizi wa ujenzi wa mradi huo. |
Mhe. Kawawa akitoa ufafanuzi kwa wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa Mahakama baada ya kukamilisha kupata taarifa ya hali ya utekelezaji wa mradi huo. |
Mhe. Jaji Sacko akimvisha Mhe. Kawawa nembo ya Mahakama hiyo ikiwa ni ishara ya shukrani kwa mchango mkubwa unaotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama katika utekelezaji wa majukumu ya Mahakama hiyo.
|
Picha ya Pamoja |
Friday, June 14, 2024
MAKATIBU WAKUU WA EAC WAFANYA MASHAURIANO KUHUSU UANZISHWAJI WA VITUO VYA UMAHIRI
Makatibu Wakuu wa sekta ya afya kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana leo, tarehe 14 Juni, 2024, jijini Arusha kwa kikao cha mashauriano.
Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa 7 wa Dharura wa Baraza la Kisekta la Mawaziri, unaotarajiwa kuitishwa katika tarehe itakayopangwa baada ya kukamilika kwa mashauriano hayo.
Mashauriano haya yanafanyika kufuatia wasilisho la pendekezo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuanzisha vituo vya umahiri, ambavyo ni Kituo cha Umahiri cha Sayansi ya Afya ya Kinywa chini ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), na Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto na Sayansi ya Matibabu ya Magonjwa ya Damu chini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa.
Akihutubia katika ufunguzi wa Mkutano huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, ameeleza kuwa kuanzishwa kwa vituo hivyo vya kikanda kutasaidia kuinua uwezo katika matibabu ya kibingwa, mafunzo ya kibobezi, utafiti, na utoaji wa huduma maalum za afya.
Aidha, amefafanua kuwa kuanzishwa kwa vituo hivyo ni ushahidi wa nia ya dhati ya kukuza ushirikiano wa kikanda, hususan katika masuala ya afya na elimu. Vilevile, vituo hivyo vitatumika kama maeneo ya kukuza ubunifu, vipaji, na utaalamu wa kikanda na katika maeneo mengine.
Naye Mwenyekiti wa kikao hicho, Katibu Mkuu wa Afya wa Jamhuri ya Sudan Kusini, Dkt. Ader Macar Aclek ambaye alishiriki mashauriano kwa njia ya mtandao ameipongeza Tanzania kwa jitihada zake za kufanikisha kuwasilisha andiko dhana la kuanzishwa kwa vituo vya umahiri. Pia, ameonyesha umuhimu wa kushirikiana katika kupambana na changamoto za kidunia, hususan mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamekuwa yakileta mlipuko wa magonjwa mbalimbali yanayohitaji jitihada za pamoja kukabiliana nayo.
Wakati huo huo, Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu, Sekta za Miundombinu, Uzalishaji, Jamii na Siasa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki alitumia wasaa huo wa ufunguzi wa kikao kuwaeleza wajumbe kuwa ana matumaini majadiliano ya kikao hicho yatafanyika kwa tija na masilahi mapana ya kikanda.
Kadhalika, alishauri kuwa ni vyema Nchi Wanachama zikatoa ushirikiano katika uanzishwaji wa vituo hivyo vipya ili viweze kufikia malengo ya utendaji yanayotarajiwa katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiafya zinazoendelea kikanda na ulimwenguni kwa ujumla.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huu wa Makatibu Wakuu umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, ambaye ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe, pamoja na maafisa waandamizi kutoka wizara na taasisi za afya na elimu nchini.
[18:15, 14/06/2024] Judith Ngoda: The EAC Permanent Secretaries held a consultative meeting at the EAC HQs in Arusha. The main agenda of the discussion was the considerations of the concept note for the two proposed EAC Regional Centers of Excellence to be hosted by the United Republic of Tanzania.
===============================
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe akiwasilisha hotuba ya ufunguzi katika kikao cha Mashauriano cha Makatibu Wakuu kilichofanyika jijini Arusha, tarehe 14 Juni, 2024. |
![]() |
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Abdillah Mataka akifuatilia majadiliano katika kikao cha Makatibu Wakuu. |
![]() |
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa kikao wa Wataalam kutoka Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhandisi Ring Rut ambaye Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka na Mkuu wa Idara ya Afya katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Eric Nzeyimana wakiongoza majadiliano ya kikao hicho. |
![]() |
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe (kulia) na Makamu Mkuu wa Chuo cha Afya Shirikishi cha Muhimbili, Prof. Bruno Sunguya wakifuatilia majadiliano ya kikao. |
![]() |
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia majadiliano. |
![]() |
Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania ukifuatilia majadiliano. |
![]() |
Ujumbe wa Tanzania. |
Thursday, June 13, 2024
WAATALAM WA SEKTA YA AFYA KUTOKA NCHI ZA EAC WAKUTANA JIJINI ARUSHA
Wataalam
wa sekta ya afya kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana
jijini Arusha katika kikao cha maandalizi ya Mkutano wa Saba (7) wa Dharura wa
Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya utakaofanyika kesho tarehe 14 Juni, 2024
na kutanguliwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu.
Mkutano
huu wa wataalamu pamoja na masuala mengine utapitia na kujadili pendekezo la Tanzania la kuanzisha vituo viwili vya umahiri ambavyo ni: Kituo cha
Umahiri cha Sayansi ya Afya ya Kinywa chini ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi
Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto na
Sayansi ya Matibabu ya Magonjwa ya Damu chini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa.
Akifungua
mkutano huo Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka ameeleza kuwa kupitia mkutano huu wajumbe
watachangia na kushauri juu ya umuhimu wa vituo hivyo viwili vya umahiri
ambavyo vinachangia utoaji wa huduma za kibingwa za afya pamoja na mafunzo katika
kanda ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Naye Mwenyekiti
wa mkutano wa Wataalam kutoka Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhandisi Ring Dut katika
hotuba yake ya ufunguzi ameeleza kuwa kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa
COVID-19 kumeleta somo katika ukanda wa Afrika Mashariki hususan katika suala
la kujijengea uwezo wa kujitegemea katika masuala ya huduma za afya, uanzishaji
wa programu saidizi na uimarishwaji wa miundombinu katika sekta hiyo.
Ujumbe
wa Tanzania katika Mkutano Ngazi ya Wataalam umeongozwa na Kaimu Mkurugenzi
Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Abdillah Mataka ambaye
ameambatana na Wataalamu Waandamizi kutoka sekta ya Afya na Elimu.
Katika hotuba yake ya ufunguzi Mhandisi amesisitiza
umuhimu wa mkutano huo, akibainisha kuwa andiko dhana ya kuanzisha vituo vya
umahiri vilivyopendekezwa na Tanzania vitaleta mabadiliko muhimu katika mifumo
ya afya, huduma za kibingwa, mafunzo, na kujengea uwezo.
Pia, amewahimiza wajumbe kujadili na kushiriki
katika mijadala ya wazi na yenye kujenga ili kuboresha afya kwa ustawi wa watu
wa EAC, huku akitoa shukrani kwa wadau wote walioshiriki katika kuandaa
maandiko haya ya dhana.
============================================
Mwenyekiti wa Mkutano wa Wataalam kutoka Jamhuri ya Sudan Kusini, Mhandisi Ring Rut (wa pili kushoto) akifungua Mkutano Ngazi ya Wataalamu kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa Saba (7) wa Dharura wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya utakaofanyika tarehe 14 Juni, 2024 jijini Arusha. Kulia kwake ni: Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka, Mkuu wa Idara ya Afya kutoka kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Eric Nzeyimana na kushoto ni Mnukuu (Rapportuer) kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Dkt. Dieumerci Kaseso. |
Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Irene Isaka (kati) akitoa hotuba ya ufunguzi katika Mkutano Ngazi ya Wataalam unaofanyika tarehe 13 Juni, 2024 jijini Arusha. |
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Abdillah Mataka akitoa neno la ufunguzi katika Mkutano Ngazi wa Wataalam unaofanyika jijini Arusha tarehe 13 Juni, 2024.
|
Ujumbe kutoka Uganda |
Ujumbe kutoka Tanzania |
Sehemu nyingine ya Ujumbe kutoka Tanzania |
Picha ya pamoja |
Monday, June 10, 2024
BALOZI MUSSA AWAASA VIJANA KUWA MABALOZI WAZURI NJE YA NCHI
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akisisitiza jambo alipokuwa akiwaaga washiriki wa programu ya mafunzo ya uongozi kwa vijana(Mandela Washington Fellowship for Young African Leaders is the flagship program)yatakayofanyika nchini Marekani. |
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akiwa katika mazungumzo na vijana waliochanguliwa kushiriki katika programu ya mafunzo ya uongozi kwa vijana (Mandela Washington Fellowship for Young African Leaders is the flagship program) kwenye hafla fupi ya kuwaaga vijana hao iliyofanyika Mtumba, jijini Dodoma. |
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akiwa katika mazungumzo na vijana waliochanguliwa kushiriki katika programu ya mafunzo ya uongozi kwa vijana (Mandela Washington Fellowship for Young African Leaders is the flagship program) kwenye hafla fupi ya kuwaaga vijana hao iliyofanyika Mtumba, jijini Dodoma. |
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akikabidhi Bendera ya Taifa kwa vijana waliochanguliwa kushiriki katika programu ya mafunzo ya uongozi kwa vijana (Mandela Washington Fellowship for Young African Leaders is the flagship program) kwenye hafla fupi ya kuwaaga vijana hao iliyofanyika Mtumba, jijini Dodoma. |
![]() |
Picha ya pamoja. |
KATIBU MKUU MAMBO YA NJE AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KIKAO CHA SADC MASUALA YA SIASA NA DIPLOMASIA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Kikao cha Pamoja cha Kamati Ndogo ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuhusu masuala ya Siasa na Diplomasia kilichofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 10 Juni 2024.
Akifungua kikao hicho ambacho kimefanyika kwa ngazi ya Makatibu Wakuu , Mwenyekiti ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Zambia, Bi. Etambuyu Gundersen aliwataka wajumbe kujadili na kutoa mapendekezo katika agenda mbalimbali zilizowasilishwa kwao ili hatimaye mapendekezo hayo yawasilishwe kwenye kikao cha Mawaziri kitakachofanyika mwezi Julai 2024 kwa ajili ya kuridhiwa.
Akichangia hoja kwenye kikao hicho, Balozi Shelukindo amezishukuru na kuzipongeza Nchi Wanachama wa SADC kwa kufanikisha uundwaji na uzinduzi wa Sanamu ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliofanyika mwezi Februari 2024 katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Amesema uzinduzi huo ambao ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wakuu wa nchi wa Afrika ulidhihirisha namna ambavyo wanaenzi mchango mkubwa uliotolewa na Hayati Mwalimu Nyerere kwenye Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika.
Kadhalika amesema Tanzania inaendelea na mawasilianao ya ndani ili kukamilisha Mpango wa Taifa wa Utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa Namba 1325 kuhusu kuwawezesha Wanawake kushiriki katika juhudi za kutatua, kuzuia na kudhibiti migogoro duniani huku akizipongeza nchi zilizokamilisha Mpango huo ikiwemo Zimbawe na Madagascar.
Vilevile, ametumia fursa hiyo kuzipongeza Jamhuri ya Afrika Kusini na Jamhuri ya Madagascar kwa kufanikisha uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge uliofanyika kwenye nchi hizo kwa amani na utulivu tarehe 29 Mei 2024 mtawalia.
Amesema, kikanda uchaguzi katika nchi hizi mbili umeakisi viwango vya kimataifa vya demokrasia pamoja na kanuni na miongozo ya SADC kuhusu uchaguzi unaofuata misingi ya demokrasia.
Kikao hicho ambacho kimefanyika kwa ajili ya kuandaa mkutano wa Mawaziri unaotarajiwa kufanyika mwezi Julai 2024, kimehudhuriwa na Nchi za Tanzania, Lesotho, Eswatini, Botswana, Angola, Namibia, Afrika Kusini, Shelisheli , Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia na Zimbabwe.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akizungumza wakati wa Kikao cha Pamoja cha Kamati Ndogo ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuhusu masuala ya Siasa na Diplomasia kilichofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 10 Juni 2024 |
Katibu Mkuu, Balozi Shelukindo akichangia hoja wakati wa Kikao cha Pamoja cha Kamati Ndogo ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuhusu masuala ya Siasa na Diplomasia kilichofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 10 Juni 2024. Kulia ni Afisa Mambo ya Nje anayeshughulikia Dawati la SADC, Bi. Shazma Msuya akinukuu taarifa ya kikao hicho. | |
Kikao kikiendelea |