Monday, June 24, 2024

WIZARA YA MAMBO YA NJE ILIVYOSHIRIKI KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) amesema maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma ambayo hufanyika tarehe 23 Juni kila mwaka yanalenga kuhamasisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi katika utumishi wa umma barani Afrika

Waziri Mkuu alisema hayo wakati wa hafla ya kufunga maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na ufunguzi wa mifumo ya kielekitroniki ya uwajibikaji katika utumishi wa umma (E-UTUMISHI) iliyofanyika juni 23, 2024 kwenye viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Taasisi za Umma ikiwemo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo ilishiriki maadhimisho hayo zilielekezwa kuhakikisha kuwa zinajiunga kwenye mifumo hiyo na kuwa na mpango endelevu wa kuwaelimisha watumishi namna ya kuitumia.

Mifumo hiyo ni pamoja na mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara (HCMIS); Mfumo wa Utumishi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma ((PEPMIS/PIPMIS), Mfumo wa Tathmini ya Rasilimaliwatu (HRA) na Mfumo wa Kushughulikia  Mrejesho wa Wananchi  kuhusu Huduma Zinazotolewa na Serikali (e-MREJESHO).

Amesema mifumo hiyo ni muhimu kwa kuwa inarahisisha na kuharikisha huduma kwa wananchi pamoja na kuondoa kero kama vile za rushwa na urasimu. 

Waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla kuchangamkia mifumo hiyo ambayo imeunganishwa na taasisi nyingine kama za huduma za kifedha, mifuko ya pensheni na Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho.

Waziri Mkuu aliwapongeza wabunifu wa mifumo hiyo ambao wote ni Watanzania kwa kubuni mifumo yenye tija na ubora mkubwa ambayo imetambuliwa na taasisi ya umoja wa mataifa ya “United Nations Public Services Awards”.

Waziri Mkuu alihitimisha hotuba yake kwa kuagiza kila Mkuu wa taasisi aweke mipango ya usimamizi na uongozi wa mifumo hiyo ili iweze kutumika kwa ufanisi katika ngazi ya taasisi yake; taasisi za umma zihakikishe usalama wa takwimu na taarifa zinazowekwa kwenye mifumo hiyo. Alisema mifumo hiyo ina taarifa muhimu na nyeti, hivyo ni muhimu kuhakikisha taarifa hizo zinalindwa ipasavyo ili kuepuka uhalifu wa kimtandao pamoja na kutoa mafunzo na kuhamasisha matumizi ya mifumo hiyo ambayo ni migeni kwa watumishi. 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo (Mb) akisaini Kitabu cha Wageni alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo (Wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea Banda la  Wizara wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.

Mwananchi akipata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu utekelezaji wa diplomasia ya Uchumi alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.
Mwananchi akihudumiwa alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.

Wananchi wakihudumiwa walipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifafanua masuala mbalimbali kuhusu utendaji wa Wizara hiyo kwa Mwananchi aliyotembelea Banda la Wizara wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2024.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.