Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Melanie Joly akizungumza na Mabalozi wa Afrika waliopo nchini humo uliofanyika hivi karibuni jijini Ottawa |
Friday, June 7, 2024
WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CANADA AKUTANA NA MABALOZI WA AFRIKA
Monday, June 3, 2024
MKUTANO WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI LINALOSHUGHULIKIA MASUALA YA EAC NA MIPANGO WAANZA ARUSHA
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Benjamini Mwesiga akichangia hoja kwenye Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha |
Mkutano ukiendelea |
Mkutano ukiendelea |
Meza kuu wakiongoza Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha |
KAMATI YA BUNGE YA NUU YASISITIZA UWAJIBIKAJI
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) imeisisitiza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi yake kwa wakati iliyo katika hatua mbalimbali.
Msisitizo huo umetolewa katika kikao cha ufuatiliaji kati ya kamati hiyo na Menejimenti ya Wizara kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma, tarehe 3 Juni 2024.
Akiwasilisha taarifa ya miradi ya ujenzi iliyo chini ya Wizara, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.), kwa niaba ya Mhe. January Makamba (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ameeleza kuwa, Wizara imewekeza nguvu kubwa katika kuhakikisha mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi ya Wizara lililopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma na jengo la mihadhara la Kituo cha Uhusiano cha Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim kilichopo Kurasini, jijini Dar es Salaam yanakamilika kwa wakati.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya NUU na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mhe. Vita Kawawa (Mb.) alieleza juu ya umuhimu wa Wizara kushirikiana na Kamati hiyo katika kutekeleza majukumu yake.
Aidha, wajumbe wa Kamati wamepongeza jitihada zilizofanywa na Wizara katika utekelezaji wa miradi na wamesisitiza weledi katika usimamizi wa matumizi ya kifedha na mikataba ya miradi ya ujenzi.
Naye Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amewashukuru wajumbe wa Kamati ya NUU kwa kuendelea kuwa chachu katika usimamizi wa miradi inayotekelezwa na Wizara. Pia, amewaalika Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea mradi wa ujenzi wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu unaotekelezwa katika eneo la Lakilaki, Arusha.
========================================
Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) wakifuatilia kikao. |
Sehemu ya Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikifuatilia kikao. |
Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikifuatilia kikao. |
Kikao kikiendelea. |
Friday, May 31, 2024
MAWAZIRI WA BIASHARA ,VIWANDA, FEDHA NA UWEKEZAJI WA EAC WAAZMIA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifuatilia mkutano |
Mkutano ukiendelea |
Mkutano ukiendelea |
TANZANIA KUJIIMARISHA KATIKA UKANDA WA IORA
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya hiyo uliofanyika kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dodoma na kuhitimishwa leo tarehe Mei 31, 2024.
Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao huku ujumbe wa Tanzania ukishiriki kutokea jijini Dodoma, Balozi Mussa amesema zipo fursa nyingi katika Jumuiya hiyo ambazo Tanzania ikijipanga itanufaika nazo ikiwemo utunzaji wa mazingira na rasilimali za bahari, ulinzi na usalama baharini, namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, uvuvi na utalii na kwamba wakati umefika sasa wa kuhakikisha wananchi wa Tanzania wananufaika kupitia jumuiya hiyo.
Aidha, kupitia mkutano huo Balozi Mussa amewasisitiza wajumbe wa mkutano waliotoka katika Taasisi, Wizara na Idara za Serikali kuendelea kuhakikisha maazimio mbalimbali yanayofikiwa kupitia Jumuiya hiyo yanatekelezwa kikamilifu ili kulinufaisha taifa kiuchumi na kijamii kwa ujumla.
“Ninawahimiza tuendelee kushirikiana ili taarifa za utekelezaji wa maazimio ya mkutano huu yaweze kufanyiwa kazi kwa haraka na kuiwezesha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kuratibu shughuli za kikanda na kimataifa kwa tija na maslahi mapana ya Nchi’’ alisema Balozi Mussa.
Kadhalika wakati wa Mkutano huo, Tanzania iliwasilisha pendekezo la Mradi kuhusu Ushirikishwaji wa Jamii za Pwani katika Utunzaji wa Rasilimali za Bahari za ukanda wa Pwani ambalo linalenga pamoja na mambo mengine kuzijengea uwezo jamii za Pwani kutunza rasilimali za bahari na kuibua fursa za kiuchumi zitakazowanufaisha na kuinua kipato cha wananchi wa ukanda wa Pwani.
Akiwasilisha pendekezo hilo, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Dkt. Saida Fundi amesema Chuo hicho kilikuja na wazo la kuandaa mradi huo baada ya kuona upo umuhimu mkubwa wa kuziwezesha jamii zilizopo kwenye mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi kunufaika na rasilimali zitokanazo na bahari.
Amesema pendekezo la mradi huo ambalo litahusisha Warsha itakayofanyika hapa nchini mwezi Oktoba 2024 na kuzihusisha nchi wanachama na wadau mbalimbali lina malengo mahsusi ikiwemo kuimarisha mtandao wa watumiaji wa rasilimali za bahari katika ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na kuzijengea uwezo jamii za ukanda wa Pwani ili kunufaika na fursa mbalimbali.
========================
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mkutano. |
Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania. |
Mkutano ukiendelea. |
UBALOZI WA TANZANIA NAMIBIA WARATIBU JUKWAA LA BIASHARA NA UWEKEZAJI
Katibu Mkuu, Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia
masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi akizungumza |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
Washiriki wa jukwaa hilo wakifuatilia akizungumza wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024 |
meza kuu katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa jukwaa hilo |
Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia umeratibu na kushiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika jijini Windhoek tarehe 30 Mei 2024.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi,ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa hilo.
Jukwaa hilo limejumuisha Sekta za Kilimo, Mifugo, Utalii, Biashara na Uwekezaji.
Thursday, May 30, 2024
MAKATIBU WAKUU SEKTA YA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE MAJI WA EAC WAKUTANA ARUSHA
Picha ya pamoja |
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka akifuatilia Mkutano |