Friday, October 19, 2012

Kamati ya NUU yatembelea Kituo cha Julius Nyerere

Jengo la Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) linavyoonekana kwa nje baada ya kukamilika. Jengo hilo linalomilikiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  lipo Makutano ya Barabara za Shaaban Robert na Garden Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule (kushoto) akimkaribisha Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb.), Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.

Katibu Mkuu, Bw. Haule akiwakaribisha Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere walipokitembelea hivi karibuni.

Wajumbe wa Kamati ya NUU na Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati akiwakaribisha.

Mhe. Azzan akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya NUU na Menejimenti ya Wizara ya Mambo ya Nje. Kulia ni Balozi Rajab Gamaha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje.

Katibu Mkuu, Bw. Haule akitoa maelezo kuhusu Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama waliotembelea kituo hicho hivi karibuni.

Thursday, October 18, 2012

Tanzania, Oman to enhance Political and Economic Ties


Tanzania and the Sultanate of Oman yesterday signed various agreements aimed at enhancing political and economic ties between the two countries.  The Agreements were signed during the second day of President Jakaya Mrisho Kikwete's State Visit to the Sultanate of Oman following the invitation of His Majesty Sultan Qaboos bin Said Al Said.

The Agreements were signed yesterday during the joint Tanzania-Oman business forum held at Al Bustan Hotel in Muscat, Oman.  They are: Agreement on Promotion and Protection of Investment, Memorandum of Understanding on Cooperation in higher Education between Oman and Zanzibar, Agreement on Cooperation in Records and Archives and the Agreement on Forming joint Business Council between Oman and Tanzania.

 
Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation exchanges legal instruments with Sultan bin Salim Al Habsi, Secretary General of the Oman Ministry of Financial Affairs.  The Agreements signed were for Promotion and Protection of Investment.  Witnessing the ceremony is H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete.


Zanzibar's Minister for Labour, Cooperatives and Economic Empowerment, Haroun Ali Suleiman and Oman Minister for Higher Education, Dr. Rawiyah Al Busaidi exchanging legal instruments on Memorandum of Understanding on Cooperation in higher Education between Oman and Zanzibar.  Witnessing the ceremony is H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania.


Mr. George Yambesi, Permanent Secretary, President's Office (Civil Service) exchanges signed legal instruments with Dr. Hamed bin Mohamed Al Dhawyan, Oman's Under Secretary at the Ministry of Heritage and Culture.  The Agreement based on Cooperation in Records and Archives.  


Mr. Aloyce Joseph Mwamanga, President of Tanzania Chamber of Commerce, Agriculture and Industry signs Agreement on Forming joint Business Council between Tanzania and Oman.  Witnessing the ocassion is Mr. Khalil Abdullah Al Konji (right- seated), Oman's President of Chamber of Commerce and Industry.



All photos by Freddy Maro (courtesy of www.issamichuzi.blogspot.com)






Wednesday, October 17, 2012

President Kikwete's keynote address in Oman Business Forum




KEYNOTE ADDRESS BY H. E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DURING THE TANZANIA – OMAN BUSINESS FORUM, MUSCAT, OMAN 16th  OCTOBER, 2012

H.E. Khalil Al Khonji, Chairman, Oman Chamber of Commerce and Industry;
Eng. Aloys J. Mwamanga, President, Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture;
Ms. Munira Humoud Said, President, Zanzibar Chamber of Commerce, Industry and Agriculture;
Honorable Ministers;
Distinguished Businessmen and Women;
Invited Guests;
Ladies and Gentlemen;

I thank you Mr. Khalil Al Khonji, Chairman of the Oman Chamber of Commerce and Industry for inviting me to attend and speak at the historic first, Tanzania – Oman Business Forum.  I thank the Oman Chamber of Commerce and Industry and the Tanzania Embassy for conceiving the idea of holding this important meeting and organizing it so well. I am visiting the Sultanate of Oman, at the invitation of His Majesty Sultan Qaboos, to consolidate the longstanding historic social, political and economic relations and cooperation that so happily exists between our two countries and peoples. This, Forum, therefore is a vehicle for promoting and strengthening economic, trading and investment cooperation between our governments and peoples. I wish events of this nature could take place more often and regularly, both here in Oman and back home in Tanzania.  

Ladies and Gentlemen;

          The Sultanate of Oman is a very special country to Tanzania. There is no other country on this planet with as many of its citizens who have blood relations with the people of Tanzania. This is a unique asset or resource which our two countries can use to promote stronger political, social and economic ties for the mutual benefit of our two countries and two peoples. I am undertaking this visit and I speak at this Forum this afternoon precisely for that reason.

Ladies and Gentlemen;

I heartily welcome the holding of this Forum and I look forward with great anticipation to the outcome of this meeting.  I hope Oman and Tanzanian business people and the several government officials   gathered here this afternoon will rise to the occasion and take our economic relations to the next level.  I want to see increased economic, investment and business relations between our two friendly countries become more robust because we both have a lot to offer to each other and much to benefit.

Ladies and Gentlemen;

          Let me start by stating emphatically that Tanzania is a great place to invest and do business.   We have worked so hard for over two decades now to put in place a very conducive investment environment.  We have opened our doors wide for anyone interested to bring capital and do business with us.  We offer a wide range of investment incentives just like several other popular investment destinations in the world.  And, in some respect we are even more generous and attractive.

I am happy that I have brought with me responsible government officials and some businessmen from both Zanzibar and Tanzania Mainland who will give you detailed information and answer all your questions.


Peace, Good Governance and Conducive Business Environment

Ladies and Gentlemen;

Tanzania is a peaceful and politically stable country. This is a critical asset for one to invest. We are a young vibrant multiparty democracy. We uphold the tenets of good governance, respect of human rights and the rule of law. The fight against corruption and other vices in society is unwavering, despite the daunting challenges we are faced with.

Private investments in Tanzania are guaranteed by   government policy and law against nationalization and expropriation. Investors are allowed to take their money.  They can repatriate profits and dividends without inhibitions.  Besides, Tanzania is a signatory and a party to several multilateral and bilateral agreements on protection and promotion of investments. Among such international agreements and memberships, Tanzania is a member of Multilateral Investment Guarantee Agency of the World Bank (MIGA) and the Swiss based International Centre for Settlement of Investment Disputes (ICSID). 

At the bilateral level, Tanzania has entered into investment promotion and protection agreements with many countries.  I am happy that, shortly before my coming here we witnessed the signing of the Agreements on the Promotion and Protection of Investment and the establishment of Joint Business Council between Oman and Tanzania. Surely, these will go a long way towards reducing further the risk of investing in Tanzania and promoting business relations. I hope our two governments will conclude at the earliest possible time, ongoing the negotiations on the avoidance of double taxation.  

Market-based Economy with Stable Macroeconomic and Fiscal Policy Regime

Ladies and Gentlemen;

Tanzania espouses market based economic policies.   This is very much a function of economic reforms we have been undertaken since the mid-1980s. As you may know, prior to that Tanzania espoused socialist policies. All commanding heights of the economy were in the hands of the state.  The state was involved in the production and distribution of goods and services from village to national level.  The state also continued to perform the traditional functions of maintaining law and order and, governing with the advent of economic reforms a fundamental policy decision was made.  This was about the government doing the primary functions of the state of governing and maintaining law and order, leaving the private sector to do business. 

Briefly, the new policy could be summarized as follows, let “Government Govern and Private Sector do Business”.  In pursuit of this new policy the government began to withdraw from direct involvement in production and distribution activities and left them in the hands of the private sector.  A comprehensive programme of divestiture   of state enterprises followed.  Todate, most state enterprises have been privatized except for a few public utilities in the sector of water, electricity, railways, roads, health and education.  Even with these sectors, the private sector is allowed direct involvements.  The government still owns the state enterprises although in some aspects there is private sector participation.  

The economic reforms have worked well for the Tanzanian economy despite some challenges.  The economy has turned around from the stresses and downward trends before the reform.  The macro-economic frame back on track and benefits are being enjoyed.  Tanzania today enjoys macro-economic stability. All macro-economic indicators are good and at the seven percent average economic growth rate over the past decade, Tanzania is among the 20 fastest growing economies in the world.  Currently, due to high food and oil prices, inflation has been a challenge.  However, there are positive signs of decline, from 19.5 percent three months ago to 14.9 percent last month.  We hope to get back to single digit by June, 2013. 

Geographical Location

Ladies and Gentlemen;
Tanzania is strategically located in the eastern coast of Africa so, come and invest to take advantage of it. Tanzania borders eight countries of Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Democratic Republic of Congo, Zambia, Malawi and Mozambique. It is a gateway for six landlocked countries Zambia, Malawi, Rwanda, Democratic Republic of Congo, Burundi and Uganda which use Tanzanian ports, roads, railways for their import and export trade. Tanzania is also the gateway for goods to and from Eastern DRC.  In this regard, therefore, investments or businesses to cater for the facilitation of imports and exports of these countries present lucrative opportunities.

One can invest in lucrative freight related businesses like clearing and forwarding, warehousing, logistic centres, trucking business etc. But there are also opportunities in port development and management, building toll roads, railways, air transportation etc.

This location also presents ample opportunities for situating manufacturing and trading businesses in Tanzania.  There is almost a captive market to take advantage off.  Fortunately, also Tanzania shares regional economic grouping with all these countries. As such, locating your businesses in Tanzania enables you to access the East African Community market of 120 million people which are in Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi.  You can also access close to 200 million people market of the Southern African Development Community, with the DRC, Zambia, Malawi, Mozambique, Angola, Namibia, South Africa, Zimbabwe, Lesotho, Swaziland, Mauritius, Seychelles and Madagascar.  In these two economic groupings there is free movement of goods and services. There is discussion going on between East African Community, SADC and COMESA of creating free Trade Area.  This boasts population of close to 540 million and USD 1trillion GDP.

Ladies and Gentlemen;

Besides its geography Tanzania itself presents abundant investment opportunities in agriculture, mining, tourism, manufacturing, fishing, ICT, and infrastructure development. In agriculture there is plenty of arable land yet to be utilized, the climate is permissive and there are adequate water resources for irrigation.  In mining nearly all minerals known to exist in the earth crust also do exist in Tanzania and some in large qualities.  Of recent, with the new discoveries of sizeable natural gas deposits, it makes Tanzania to be a prospective an emerging market for gas production in the world.  

In the hospitality industry with the beautiful and historic spice Islands of Zanzibar and exotic world renown game parks, on the mainland. Tanzania is a tourist destination worthy investing now and in future. With the huge lakes and 1000 km of sea coastline and the 200 km EEZ, fishing is a highly prospective investment opportunity.  Right now there is no serious fishing in our sea.

There are limitless opportunities in infrastructure development, telecommunications, power generation, railways, ports development, airports, airlines etc. With a huge raw material base from agriculture, mining, fishing and forestry investments in manufacturing present huge potential.  There is, as mentioned earlier, a sizeable own market of close to 45 million people, 120 million people East African Community and 200 million people of SADC market. But we also have market access arrangements with the USA under AGOA, European Union (Everything but arms), China and Japan which makes investing in Tanzania even more attractive.

Skilled Labour Force

Ladies and Gentlemen;
Tanzania, also boasts of having sizeable population of skilled labour force. Over the years, we have invested substantially in education at all levels, from primary to secondary school and higher learning. We have also expanded vocational education and established training centres in every region of the country. These have been useful in training highly qualified experts in many fields as well as technicians and artisans in various trades. While we have invested heavily in education to develop the local talent, we are keen on working with businesses on innovative ways to develop the local talent that is relevant to the specialized areas of interest. It is important to note also that labour in Tanzania is relatively less expensive compared to many other parts of the world.

Ladies and Gentlemen;

          The business climate that I have just described has already attracted growing number of foreign and local investors from different countries to Tanzania. Oman is also included in that list as between 2000 to 2011, Omani investors have registered 36 projects worth more than USD 200 million in different sectors. This is not much compared to what can be availed by Omani business community. We look forward to increased  investments because as I mentioned, opportunities are many. The returns are good, protection is guaranteed and incentives are really competitive. We also look forward to increasing trade between Tanzania and Oman, which is currently very low.

          So I warmly welcome you to come to Tanzania and explore the unlimited, trade, investment and business opportunities which our country has to offer.

Ladies and Gentlemen;

          Those interested in investing in the manufacturing business can take advantage of the opportunities which exist in the various Export Processing Zones (EPZ) and the Special Economic Zones (SEZ) which we have set up to promote and facilitate industrial development and export of manufactured goods to the worlds.  We cannot continue to be exporter of raw materials.  We want to add value to our primary products.  We will support all those of you who will opt to operate in these designated zones.

Ladies and Gentlemen;

          Let me conclude by saying the following.  First, Tanzania meaning both Zanzibar and Tanzania Mainland is ready to do business with you. Our doors are wide open.  Secondly, Tanzania have everything that you need to look for in taking a decision about where to invest: conducive business environment, political sound economic policies, macro-economic stability, abundant natural resources, relative educated labour-force, a sizeable and captive market because of Tanzania’s  unique geographical location. Above all, the government is facilitative.  The list is long, I can hardly exhaust it. As mentioned earlier these will be elaborated further in the course of your discussions by the representatives of the Tanzania Investment Centre (TIC) and the Zanzibar Investment Promotion Authority (ZIPA) who are here with us. 

Several ministers are also here to clarify on some of these issues and concerns. Above all, business men and women from Tanzania are also here to share their experiences and expectations.
         
       After those many words, I declare the Tanzania – Oman Business Forum is officially open. I thank you for listening and wishing you very successful deliberations.

Thank you very much and God bless you.




Mhe. Balozi Maajar akutana na Watanzania mjini Iowa‏



Mhe. Balozi Mwanaidi Sinare Maajar (kulia), Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watanzania (Singo na Godlisen) waliokutana naye kwenye Chuo Kikuu cha Des Moines Jimboni Iowa kabla ya kuanza Mkutano wa Iowa - Tanzania mjini Des Moines tarehe 16 Oktoba, 2012.

Mhe. Balozi Mwanaidi Sinare Maajar (kushoto) akisalimiana na Dkt. Allan Hoffman, Rais Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Santa Barbara, Carlifornia ambaye naye alijumuika na Watanzania kwenye mazungumzo hayo na Balozi Maajar kabla ya Mkutano wa Iowa - Tanzania kuanza.


Rais wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ijulikanayo kama Empower Tanzania, Bw. Phil Latesa akizungumza na Dkt. Allan Hoffman na Bw. Singo baada ya mkutano na Mhe. Balozi Maaar (hayupo pichani).


Mhe. Balozi Mwanaidi Maajar akisalimiana na Watanzania waishio Des Moines Iowa.


Mhe. Balozi Maajar akiwa katika picha na Bw. Singo, alipokutana na Watanzania kabla ya kuhudhuria Mkutano wa II wa Iowa – Tanzania pembezoni mwa Mkutano Mkuu wa Chakula ujulikanao kama World Food Prize unaoendelea mjini Des Moines, Iowa. 


Mhe. Balozi Mwanaidi Sinare Maajar akiwa katika picha ya pamoja na Bi. Mindi Kasiga (kulia), Afisa Mwandamizi (Mawasiliano) katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico kabla ya kuhudhuria Mkutano wa II wa Iowa – Tanzania pembezoni mwa Mkutano Mkuu wa Chakula ujulikanao kama World Food Prize unaoendelea mjini Des Moines, Iowa.


Picha na habari kutoka kwa Mindi Kasiga, Ubalozi wa Tanzania - Washington, DC.





Mhe. Balozi Maajar akutana na Watanzania mjini Iowa‏

Des Moines, Iowa
16 Oktoba, 2012

BALOZI wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Mwanaidi Sinare Maajar amewaasa Watanzania waishio Jimbo la Iowa mjini Des Moines kujitokeza na kutoa maoni yao kuhusu suala la uraia wa nchi mbili kwenye mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea nchini.
Balozi aliyasema hayo alipokutana na Watanzania hao kabla ya kuhudhuria Mkutano wa II wa Iowa – Tanzania pembezoni mwa Mkutano Mkuu wa Chakula ujulikanao kama World Food Prize unaoendelea mjini Des Moines, Iowa.
Alitoa mfano wa kwake binafsi alipokuwa mwanasheria na mwanaharakati ambapo kupitia taasisi mbalimbali walifanikiwa kushawishi na hatimaye kubadilisha sheria zilizowabana wanawake kuwa na haki sawa na wanaume nchini Tanzania.
“Hakuna ushawishi mzuri kama ule unaotoka kwenu nyie wenyewe Wana Diaspora, kwani nyie ndio mliovaa kiatu cha uraia wa nchi mbili na mnajua kinabana wapi” alisisitiza Balozi na kuwaomba wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao sasa wakati muda unaruhusu kufanya hivyo.
Aliongeza kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba amethibitisha ugumu uliopo kwa wajumbe wa tume hiyo kusafiri nje ya nchi kukusanya maoni, hivyo aliwataka Watanzania waishio nje ya nchi watembelee tovuti ya mabadiliko ya katiba na kutoa maoni yao http://www.katiba.go.tz
Sambamba na kutoa maoni, Mhe. Maajar aliwaasa Watanzania wa Des Moines kujipanga ili kuunda umoja wa Watanzania ili waweze kushughulikia masuala yanayowahusu kwa pamoja. Alisema Marekani ni nchi kubwa na Watanzania waishio majimbo mengine wameitikia wito huo na sasa kuna Jumuiya za Watanzania kwenye majimbo mengi nchini Marekani.
“Kwenye jimbo hili, ni muhimu sana kuwa na Jumuiya madhubuti ili kutumia fursa hii inayojitokeza kila mwaka ya Mkutano wa World Food Prize, kukutana na viongozi wanaokuja kutoka nyumbani au hata sisi kutoka ubalozini” alihimiza.
Kwa upande wao, Watanzania waishio mjini hapa walimshukuru Balozi Maajar kwa kukutana nao na kuahidi kutekeleza yale yaliyoongelewa. Pia walipendekeza ubalozi wa Tanzania Washington D.C. ujaribu kuboresha njia za mawasiliano ya kisasa kama vile Facebook na Tweeter ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi ambao kutokana na kubanwa na kazi, hawapati nafasi ya kutembelea tovuti ya ubalozi.
Mhe. Balozi yupo mjini Des Moines, IA kwa siku mbili ambapo baadaye leo atahutubia Mkutano wa II wa Iowa – Tanzania kama mgeni rasmi ulioandaliwa na Empower Tanzania, Taasisi isiyo ya Kiserikali yenye makao makuu yake hapa Des Moines, Iowa. Kesho tarehe 17 Oktoba 2012, ataendesha mjadala wa Kukata Njaa kabla ya kuhudhuria ufunguzi rasmi wa Mkutano huu wa World Food Prize.

Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 67 ya Umoja wa Mataifa yazinduliwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa ambayo kilele chake ni tarehe 24 Oktoba, 2012. Maadhimisho ya kilele yatafanyika jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Karimjee.
Wengine katika picha, aliyekaa ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Alberic Kacou na aliyesimama pembeni mwa Katibu Mkuu ni Bw. Songelaeli Shilla, Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katikaWizara ya Mambo ya
Nje.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Alberic Kacou (kushoto) akielezea umuhimu wa maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani). Kulia ni Bw. John M. Haule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Baadhi ya Waandishi kutoka Vyombo mbalimbali vya Habari wakimsikiliza kwa makini Bw. Kacou (hayupo pichani).

Menejimenti ya Wizara yatembelea Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere

Jengo la Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) linavyoonekana baada ya kukamilika. Kituo hiki kinachomilikiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kimejengwa Jijini Dar es Salaam kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

Moja ya Kumbi za Mikutano katika Kituo hicho.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M.Haule (kulia) akifafanua jambo kwa baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara wakati ujumbe huo ulipotembelea Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

Katibu Mkuu (mwenye suti) akimsikiliza kwa makini Bi. Bertha Lynn, mmoja wa Wataalam walioshiriki katika ujenzi wa Kituo hicho kutoka China alipokuwa akifafanua jambo.Wengine katika picha ni Bw. Huang Mei Luan (kushoto kwa Katibu Mkuu), Mkurugenzi wa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho kutoka China na Bw. Isaya Kapakala, Afisa anayesimamia mradi huo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M.Haule akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara na Wataalam wa Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

Monday, October 15, 2012

Balozi wa Japan hapa nchini aongoza ujumbe kuonana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifafanua jambo kwa wageni waliofika kumtembelea Ofisini kwake leo. Kulia kwa Balozi Kairuki ni Mhe. Masaki Okada, Balozi wa Japan hapa nchini akifuatiwa na Bw. Yoshiyasu Mizuno, Mshauri wa masuala ya Maendeleo ya Viwanda kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara ya hapa nchini. Anayewatazama ni Bw. Takuya Osada kutoka Kampuni ya Global Business Division ya Japan.

Balozi Kairuki (katikati) akiwa na Balozi Okada (kushoto) na Bw. Mizuno wakimsikiliza Bw. Takuya (hayupo pichani) wakati ujumbe huo ulipofika kumtembelea Balozi Kairuki Ofisini kwake leo.

Bw. Takuya akimsikiliza kwa makini Balozi Kairuki (hayupo pichani) alipokuwa akimweleza masuala mbalimbali baada ya kumtembelea ofisini kwake. Anayendika ni Afisa kutoka Ubalozi wa Japan hapa nchini.


Balozi Kairuki akifurahia jambo na Bw. Mizuno wakati wa kuagana baada ya mazungumzo yao.

Mkurugenzi wa Asia akutana na Mwakilishi wa Heshima wa Australia hapa nchini

Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Ofisini kwake Bw. Thiery Murcia, Mwakilishi wa Heshima wa Australia hapa nchini alipomtembelea leo.

Balozi Kairuki akiwa katika mazungumzo na Bw. Murcia.

Balozi Kairuki akimsikiliza kwa makini Bw. Murcia alipokuwa akizungumza nae.

Balozi Kairuki akipitia moja ya nyaraka muhimu alizokabidhiwa na Bw. Murcia wakati wa mazungumzo yao.

Saturday, October 13, 2012

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Ireland hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Fionnuala Gilsenan, Balozi mpya wa Ireland hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Mhe. Balozi Gilsenan, Bibi Grace Shangali, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Anayeshuhudia pembeni mwa Bibi Shangali ni Bi. Felista Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo. Pembeni mwa Balozi ni Bw. Nicholas Michael, Afisa katika Ubalozi wa Ireland hapa nchini.

Mhe. Balozi Gilsenan akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais.

Mhe. Balozi Gilsenan akisikiliza na kufurahia wimbo wa Taifa lake ulipokuwa ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Wengine katika picha kulia kwa Balozi ni Bw. Shaaban Gurumo, Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule, Kaimu Mkuu wa Itifaki.

Mhe. Balozi Gilsenan akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi, Inspekta Billy Kachalle mara baada ya kumaliza kupiga nyimbo za mataifa ya Tanzania na Ireland kwa heshima ya Balozi huyo.