Wednesday, October 17, 2012

Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 67 ya Umoja wa Mataifa yazinduliwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa ambayo kilele chake ni tarehe 24 Oktoba, 2012. Maadhimisho ya kilele yatafanyika jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Karimjee.
Wengine katika picha, aliyekaa ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Alberic Kacou na aliyesimama pembeni mwa Katibu Mkuu ni Bw. Songelaeli Shilla, Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katikaWizara ya Mambo ya
Nje.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Alberic Kacou (kushoto) akielezea umuhimu wa maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani). Kulia ni Bw. John M. Haule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Baadhi ya Waandishi kutoka Vyombo mbalimbali vya Habari wakimsikiliza kwa makini Bw. Kacou (hayupo pichani).

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.