Wednesday, October 17, 2012

Menejimenti ya Wizara yatembelea Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere

Jengo la Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) linavyoonekana baada ya kukamilika. Kituo hiki kinachomilikiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kimejengwa Jijini Dar es Salaam kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

Moja ya Kumbi za Mikutano katika Kituo hicho.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M.Haule (kulia) akifafanua jambo kwa baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara wakati ujumbe huo ulipotembelea Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

Katibu Mkuu (mwenye suti) akimsikiliza kwa makini Bi. Bertha Lynn, mmoja wa Wataalam walioshiriki katika ujenzi wa Kituo hicho kutoka China alipokuwa akifafanua jambo.Wengine katika picha ni Bw. Huang Mei Luan (kushoto kwa Katibu Mkuu), Mkurugenzi wa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho kutoka China na Bw. Isaya Kapakala, Afisa anayesimamia mradi huo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M.Haule akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara na Wataalam wa Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.