Friday, October 5, 2012

Hafla ya Kumuaga Balozi wa Cuba hapa Nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akihutubia wakati wa hafla ya kumuaga Balozi wa Cuba aliyemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ernesto Gomez Diaz. Hafla hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Double Tree, Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Cuba aliyemaliza muda wake hapa nchini, Mhe. Ernesto Gomez Diaz naye akizungumza machache wakati wa hafla hiyo.

Mhe. Naibu Waziri akiwa na baadhi ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo. Walio pembeni ya Mhe. Naibu Waziri, kulia ni Mhe. Juma Mpango, Mkuu wa Mabalozi na kushoto ni Mhe. Diaz, Balozi anayeondoka.

Mhe. Balozi Diaz akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na Mhe. Naibu Waziri.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Grace Shangali akitoa neno la ufunguNzi wa hafla ya kumuaga Balozi wa Cuba.

Mhe. Naibu Waziri akiagana na Balozi Diaz mara baada ya hafla kumalizika.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.