Saturday, October 13, 2012

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Korea hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisubiri kupokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Chung IL, Balozi mpya wa Jamhuri ya Korea hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Mhe. Balozi  IL mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho za Balozi huyo. Kulia kwa BaLozi IL ni mkewe Bibi Junghwa Moon.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi IL na mkewe Bibi Junghwa Moon mara baada ya kupokea Hati za Utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Balozi IL akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.

Mhe. Balozi IL akisikiliza Wimbo wa Taifa lake uliokuwa ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Wengine katika picha ni Bw. Shaaban Gurumo (kulia kwa Balozi) ambaye ni  Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule (kushoto kwa Balozi), Kaimu Mkuu wa Itifaki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.