Saturday, October 13, 2012

Mhe. Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Ireland hapa nchini

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Fionnuala Gilsenan, Balozi mpya wa Ireland hapa nchini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam jana.

Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Mhe. Balozi Gilsenan, Bibi Grace Shangali, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Anayeshuhudia pembeni mwa Bibi Shangali ni Bi. Felista Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo.

Mhe. Rais Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Gilsenan mara baada ya kupokea hati za utambulisho za Balozi huyo. Pembeni mwa Balozi ni Bw. Nicholas Michael, Afisa katika Ubalozi wa Ireland hapa nchini.

Mhe. Balozi Gilsenan akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais.

Mhe. Balozi Gilsenan akisikiliza na kufurahia wimbo wa Taifa lake ulipokuwa ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Wengine katika picha kulia kwa Balozi ni Bw. Shaaban Gurumo, Mnikulu na Bw. Japhet Mwaisupule, Kaimu Mkuu wa Itifaki.

Mhe. Balozi Gilsenan akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi, Inspekta Billy Kachalle mara baada ya kumaliza kupiga nyimbo za mataifa ya Tanzania na Ireland kwa heshima ya Balozi huyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.