Monday, October 15, 2012

Balozi wa Japan hapa nchini aongoza ujumbe kuonana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifafanua jambo kwa wageni waliofika kumtembelea Ofisini kwake leo. Kulia kwa Balozi Kairuki ni Mhe. Masaki Okada, Balozi wa Japan hapa nchini akifuatiwa na Bw. Yoshiyasu Mizuno, Mshauri wa masuala ya Maendeleo ya Viwanda kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara ya hapa nchini. Anayewatazama ni Bw. Takuya Osada kutoka Kampuni ya Global Business Division ya Japan.

Balozi Kairuki (katikati) akiwa na Balozi Okada (kushoto) na Bw. Mizuno wakimsikiliza Bw. Takuya (hayupo pichani) wakati ujumbe huo ulipofika kumtembelea Balozi Kairuki Ofisini kwake leo.

Bw. Takuya akimsikiliza kwa makini Balozi Kairuki (hayupo pichani) alipokuwa akimweleza masuala mbalimbali baada ya kumtembelea ofisini kwake. Anayendika ni Afisa kutoka Ubalozi wa Japan hapa nchini.


Balozi Kairuki akifurahia jambo na Bw. Mizuno wakati wa kuagana baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.