Friday, May 9, 2014

Matukio mbalimbali ya ziara ya kikazi ya Mhe. Membe nchini Uturuki


Waziri Mkuu wa Uturuki, Mhe. Recep Tayyip Erdogan (kulia) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe (Mb). mazungumzo hayo yalifanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu mjini Ankara, Uturuki tarehe 08 Mei, 2014.
Mazungumzo yanaendelea kati ya Waziri Mkuu wa Uturuki (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania. Mwingine katika picha ni Bibi Victoria Mwakasege, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Waziri Membe kulia akishikana mkono na Waziri Mkuu wa Uturuki mara baada ya viongozi hao kumaliza mazungumzo. 

Mazungumzo kati ya Waziri Membe na Waziri na Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki 

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa aliyevaa shati la njano kulia ukiwa katika mazungumzo na ujumbe wa Uturuki unaongozwa na Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler wa tatu kutoka kushoto. 

Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernard K. Membe akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki
Waziri Membe naye akimpa zawadi ya kinyago Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki 
Mhe. Membe na Naibu Waziri Mkuu wa Uturuki wakijadili suala baada ya zoezi la kukabidhiana zawadi kukamilika


Mazungumzo ya Waziri Membe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe wa tatu kutoka kushoto na ujumbe wakijadili masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano na Uutruki na ujumbe wa Uturuki unaonekana katika picha ya chini.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu wa pili kutoka kulia akiwa na ujumbe wake wakati wa mazungumzo na Mhe. Membe.

Mkutano na Waandishi wa Habari


Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mhe. Bernard K. Membe akihutubia Mkutano wa Waandishi wa Habari huku akimshika mkono Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Almet Dovutoglu
Waziri Membe akiendelea kuwahutubia waandishi wa habari hawapo pichani


Mapokezi ya Mhe. Membe nchini Uturuki


Waziri Membe akipeana mikono na watu waliofika Uwanja wa Ndege wa Ankara kumpokea
Waziri Membe kushoto akibadilishana mawazo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania katika Chumba cha Wageni Maalum kwenye Uwanja wa Ndege wa Ankara
Waziri Membe akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia ambaye pia anawakilisha Uturuki aliyekaa kushoto pamoja na Bw. Salvator Mbilinyi, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia aliyechutama wakibadilishana machache katika Chumba cha Wageni Maalum ndani ya Uwanja wa Ndege wa Ankara.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana na Naibu Meya wa jiji la Ankara ambaye naye alikuja Uwanja wa Ndege kumlaki


Naibu Meya wa jiji la Ankara aliyeketi kushoto akibadilishana mawazo na Mhe. Membe kabala ya kuondoka kutoka katika kiwanja hicho

Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania, Bw. Frank Muhina akiwa kazini kunukuu mambo mbalimbali kutoka kwa Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki. 



Na Ally Kondo, Uturuki

 WATURUKI WAHIMIZWA KUWEKEZA TANZANIA

Waturuki wenye mitaji wamehimizwa kuja Tanzania kuchangamkia fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Uturuki tarehe 08 na 09 Mei, 2014.
Katika ziara hiyo, Waziri Membe aliweza kuonana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Kitaifa wa Serikali ya Uturuki akiwemo Waziri Mkuu, Mhe. Recep Tayyip Erdogan; Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler; Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Ahmet Dovutoglu na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Lutfi Elgan.
Aidha, Mhe. Waziri na mwenyeji wake, Mhe. Dovutoglu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi habari pamoja na kushiriki chakula cha mchana na wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki.  
Mhe. Waziri alieleza kuwa Tanzania ina fursa nyingi za uwekezaji ambazo hazijatumiwa ipasavyo, hivyo ni muda muafaka kwa Waturuki kuwekeza mitaji yao nchini Tanzania kwa faida ya pande zote.
Baadhi ya maeneo ambayo yatakuwa na faida kubwa endapo yatapata wawekezaji ni pamoja na sekta ya usafiri wa anga. Hivyo,  Mhe. Waziri alilihamasisha Shirika la Ndege la Uturuki kuangalia uwezekano wa kuingia ubia na Shirika la Ndege la Tanzania. “Endapo Shirika la Ndege la Tanzania litapata mwekezaji, likawa na ndege za kutosha na kwa sababu Tanzania imezunguukwa na nchi nyingi, wasafiri wengi wa nchi hizo, watatumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuunganisha safari zao kwenda nchi za Ulaya”. Mhe. Membe alisikika akiwambia Viongozi wa Uturuki pamoja na wafanyabiashara wakubwa
Waziri Membe pia aliwahahakishia wawekezaji wa Uturuki watakaokuwa na dhamira ya kuwekeza nchini, kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA) itatoa eneo maalum ili wawekezaji hao waweze kujenga viwanda vya uzalishaji. Alisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika viwanda vya nguo, mbolea, gesi, zana za kilimo, miundombinu ya umwagiliaji, umwagiliaji wa matone  pamoja na viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, nyama na maziwa. Alisema endapo sekta hizo zitafanyiwa kazi ipasavyo basi ukuaji wa uchumi utaenda sambamba na ustawi wa maisha ya watu wa kawaida, kwa sababu sekta hizo zitaongeza ajira kwa maelfu ya vijana wa Tanzania.
Aliendelea kueleza kuwa ili ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki uendelee kuimarika, Serikali itatimiza ahadi yake ya kufungua Ubalozi nchini Uturuki katika mwaka wa Fedha 2014/2015.
Kwa upande wao, Viongozi wa Uturuki walimuhakikishia Mhe. Membe kuwa watawahamasisha wafanyabiashara wa Uturuki kuja kuwekeza Tanzania. Walisema kazi hiyo kwao ni nyepesi na wanahakika itapokelewa vizuri na jumuiya ya wafanyabiashara kwa sababu Tanzania mbali na kuwa na fursa nyingi, pia  ina utulivu wa kisiasa ambao ni kigezo muhimu katika uwekezaji. 
Katika hatua nyingine, Mhe. Membe aliishukuru Serikali ya Uturuki kwa kitendo chake cha kukubali wanamichezo 10 wa Tanzania kuweka kambi ya mafunzo kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Scotland mwezi wa Julai, 2014.
Sanjari na shukrani hizo, alimshukuru pia Balozi wa Uturuki nchini Tanzania na Mke wake kwa jitihada zao za kunusuru maisha ya watu wenye ualbino. Alisema uamuzi wao wa kujenga kijiji ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchukuwa watu wenye ualbino 500 kwa ajili ya kuwapa elimu na stadi nyingine za maisha ni mfano wa kuigwa na jamii ya wasamalia wema.  
Vile vile, Mhe. Waziri aliishukuru Uturuki kwa kulisaidia Shirika la Utangazaji la Taifa Tanzania (TBC)  kwa kulipa vifaa na teknolojia ya kisasa. Alisema kabla  ya msaada huo, TBC ilikuwa inafanya kazi katika mazingira magumu.


Thursday, May 8, 2014

Naibu Waziri aongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye uchaguzi Afrika Kusini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya wakielekea kwenye moja ya Vituo vya kupigia kura wakati wa  Uchaguzi Mkuu wa Rais nchini humo uliofanyika tarehe 7 Mei, 2014. Mhe. Dkt. Maalim anaongoza ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi  kutoka Tanzania kama nchi mwanachama wa SADC na pia  mjumbe wa Asasi ya Ulinzi, Siasa na Usalama ya SADC. 


Mhe. Dkt. Maalim akiwa na Waangalizi wengine kwenye moja ya vituo vya kupigia kura mjini Pretoria kabla ya zoezi la upigaji kura kuanza.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waangalizi wa Uchaguzi kwenye Kituo cha Taifa cha Kuratibu Matokeo. Kwa nyuma ni screen zinazoonesha matokeo kutoka sehemu mbalimbali za nchi yanavyoingia.

Press Release

H.E. Vladimir Putin, President of the Russian Federation.

PRESS RELEASE


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E. Vladimir Putin, President of the Russian Federation on the occasion of the National Day of Russia –Victory Day, on 9th May 2014. The message reads as follows:

“H.E. Vladimir Putin,
President of the Russian Federation,  
Moscow

RUSSIA


Your Excellency and Dear Colleague,

On the occasion of the celebration of your country’s National Day, I would like to convey to you and through you to the Government and people of Russia my most heartfelt congratulations.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries. On this historic day, I take this opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Russia”.


Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation,Dar es Salaam

08th May 2014








Wednesday, May 7, 2014

Press Release


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency MiloÅ¡ Zeman, President of the Czech Republic on the occasion of his country’s Liberation Day on the 8th May.

The message reads as follows;

“His Excellency MiloÅ¡ Zeman,
 President of the Czech Republic,
 Prague,

 CZECH REPUBLIC.


Your Excellency,

        On behalf of the people and government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I wish to convey my sincere congratulations to you, the people and the government of Czech Republic on the occasion of the Liberation Day of Czech Republic.

Tanzania values the close ties of friendship and co-operation and the warm and friendly relations between our two countries and the people.

I am confident that with the good will and understanding on both sides, the bilateral relations between Tanzania and Czech will continue to flourish as both countries pursue the shared ideas and objectives for the benefit of the two countries and peoples.

Please accept, your Excellency, my best wishes for your personal good health and peace and prosperity for the people of Czech Repulic”.

Issued by:  Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation of the United Republic of Tanzania, Dar es Salaam.

7th May, 2014


Tuesday, May 6, 2014

Waziri Membe Ziarani Uturuki



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



 Waziri wa Mambo   ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) atafanya ziara ya kikazi ya siku tatu nchini Uturuki kuanzia tarehe 07 – 09 Mei, 2014 kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Mhe. Ahmet Davutoglo. Madhumuni ya ziara hiyo ni kukuza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki ambao umedumu kwa kipindi kirefu sasa.

Aidha, katika ziara hiyo Mhe. Membe na mwenyeji wake watajadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki hususan, katika maeneo ya vipaumbele yaliyoainishwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Afrika na Uturuki uliofanyika mwaka 2008. 

Maeneo hayo ni pamoja na biashara, uwekezaji, kilimo, mawasiliano, afya, elimu pamoja na amani na usalama.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri ataonana na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa Uturuki akiwemo mwenyeji wake, Mhe. Davutoglo; Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Emrullah Isler; Waziri wa Uchukuzi, Usafiri wa Majini na Mawasiliano, Mhe. Lutfi Elvan; Waziri wa Nishati na Maliasili, Mhe. Tarrer Yildiz pamoja na kuongea na wafanyabiashara wa Uturuki.

Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri atafuatana na viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa; Wizara ya Viwanda na Biashara; Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika; Mamlaka ya Majengo Tanzania na Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA).

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es salaam.
 6 Mei 2014.
  

Friday, May 2, 2014

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje washiriki Sherehe za Mei Mosi

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakisheherekea Siku ya Wafanyakazi Duniani, iliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "UTAWALA BORA UTUMIKE KUTATUA KERO ZA WAFANYAKAZI"

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa kati maandamano
Maandamano yakiwa yameshika kasi
Maandamano yakiendelea
Rais wa Jamhuri ya Muungano akiwapungia mkono Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani) walipopita kwa heshima mbele yake.
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakiwa wamejawa na furaha na bashasha.





Picha na Reginald Philip

Press Release

PRESS RELEASE


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to to H.E. BronisÅ‚aw Komorowski, President of Poland on the occasion of the National Day of Poland –Constitutional Day, on 3rd May 2014. The message reads as follows:

President of Poland
Warsaw

POLAND


Your Excellency and Dear Colleague,

On behalf of the people of Tanzania and on my own behalf, I would like to extend to you and through you to the Government and people of Poland my heartfelt congratulations on the occasion of your country’s National Day.

Tanzania cherishes the good relations and co-operation that happily exist between our two countries.  On this historic day, I take the opportunity to reaffirm my country’s commitment and desire to continue working with you and your Government in strengthening further the existing ties of friendship and co-operation for the mutual benefit of our two countries and peoples.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of Poland”.


Issued by: Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam.

02nd May 2014


Tuesday, April 29, 2014

Waziri Membe akabidhi Bendera ya Taifa kwa wanamichezo wanaokwenda nje kwa maandalizi ya michezo ya Madola

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwakabidhi wawakilishi wa wanamichezo wapatao 50 wanaokwenda Nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, Scotland  mwezi Julai 2014 huku Mkurugenzi wa Michezo katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bw. Leonard Thadeo, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki na Bw. Filbert Bayi wakishuhudia.
Waziri Membe akizungumza na wanamichezo (hawapo pichani) huku Bw. Thadeo katikati na Bw. Bayi wakisikiliza.
Baadhi ya Wanamichezo wanaokwenda China, New Zealand, Ethiopia na Uturuki wakimsikiliza Mhe. Waziri Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao.
Waziri Membe akiendelea kuzungumza na wanamichezo hao. Kulia kwake ni Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Wengine  ni Mkurugenzi wa Michezo Bw. Leornard Thadeo, akifuatiwa na Bw. Philibert Bayi (wa kwanza kulia).
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Bw. Ally Mkumbwa pamoja na Afisa Mambo ya Nje Bw. Imani Njalikai wakimsikiliza Waziri Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yake na wanamichezo 
Waziri wa Mambo ya Nje akiwa katika Picha ya pamoja na viongozi na wadu mbalimbali wa michezo.
Picha na Habari na Reginald Philip



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb) Leo amewataka wanamichezo wa kitanzania kujituma na kuweka bidii katika michezo ili kufanikiwa kunyakua medali za dhahabu na kuiletea sifa Tanzania.

Mhe. Membe ameyasema hayo leo tarehe 29 Aprili, 2014 wakati akikabidhi Bendera ya Taifa kwa wamichezo  wapatao 50 wanaokwenda Nje ya Nchi kwa ajili ya Maandalizi ya Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, Scotland mwezi Julai, 2014. 

Wanamichezo hao ambao watakwenda katika nchi za China, Uturuki, New Zealand na Ethiopia wanashiriki michezo mbalimbali ikiwemo riadha, judo, kuogelea , mpira wa mezani, ngumi za ridhaa na mieleka.  

Wakati wa mazungumzo hayo ambayo yalihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Idara ya Michezo katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bw. Leonard Thadeo,  Waziri Membe alisema kuwa anaamini kwamba endapo vijana hao watajituma kwenye mazoezi na michezo wataweza kupata medali na kuiletea sifa Tanzania.

“Mtakapokuwa huko mnatakiwa kujituma kwa bidii sana, na kuweza kufanikiwa kunyakua medali za dhahabu, nawapeni changamoto ya kufanya vizuri katika michezo hiyo, kwa maana kwa kufanya vizuri mtaitangaza nchi yetu na kutuletea wafadhili wengi katika michezo”, alisisitiza Mhe. Membe.

Aidha, aliwaambia kwamba mbali ya kujitangaza, pia kwa kushinda kwao kutailetea heshima nchi yetu ambapo alitoa mfano wa Mkimbiaji wa riadha wa zamani wa Tanzania, Bw. Philibert Bayi, ambaye kwa kufanya kwake vizuri kumeifanya nchi ya Tanzania kujulikana hadi sasa.

Mhe. Membe alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana hao kujiepusha na vitendo viovu watakapo kuwa kwenye mafunzo hayo, aliwasisitiza na kuwaambia “Hakuna kisicho wezekana”.

Waziri Membe aliwaambia wanamichezo hao kwamba endapo atapata nafasi atajumuika nao wakati wa kuelekea kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola Glasgow, Scotland hapo mwezi Julai, 2014.

Awali akizungumza wakati wa mkutano huo, Rais wa Chama cha Riadha Tanzania, Bw. Anthony Mataka aliipongeza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kupitia mpango wake wa Diplomasia ya Michezo ambayo imewawezesha wanamichezo hao kupata nafasi za kwenda kujifua tayari kwa kushiriki michezo ya Madola. “Nachukua nafasi hii na kwa namna ya pekee kumshukuru Mhe.Membe na Wizara yake kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha michezo nchini inafanikiwa kupitia Diplomasia ya Michezo,” alisema Bw. Mataka.
 

Press Release

PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty King Willem-Alexander of the Kingdom of the Netherlands on the occasion of His Majesty’s Birthday.
                                              
        The message reads as follows:-

  “Your Majesty King Willem-Alexander R.,
   King of the Kingdom of the Netherlands,
   The Hague,
   THE NETHERLANDS.
 
Your Majesty,
              
It is my great pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to congratulate Your Majesty on the occasion of your 47th birthday.
                 
As you celebrate your birthday let me take this opportunity to express my deep appreciation for the excellent bilateral relations that exist between our two countries and peoples. I reiterate my personal commitment and that of my Government to working with You and Your Government in strengthening further the long, close and historic relations for common aspirations.
                   
                    Please accept Your Majesty, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of the Kingdom of the Netherlands”.


Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation,
Dar es Salaam.

29th April, 2013


Saturday, April 26, 2014

Sherehe za miaka 50 ya Muungano zafana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua  Gwaride Maalum lililoandaliwa kwa ajili ya sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika  na Zanzibar zilizofanyika kwenye Viwanja vya Uhuru jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2014.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Rais wa Uganda Kaguta Yoweri Museveni huku Mfalme Mswati wa Swaziland, Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein wakishuhudia tukio hilo. 
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (aliyenyoosha kidole) akimwonesha kitu Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe wakati wa sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 Kikosi cha Makomando wakionesha mbele ya Mhe. Rais, wageni waalikwa na wananchi mafunzo waliyopitia.
Moja ya zana za  kivita za kisasa zikipitishwa mbele  ya Mhe. Rais Kikwete na wageni waalikwa ikiwa ni moja ya kusherehea miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Ndege za kivita nazo zikipita angani .
Mwanajeshi akitua na mwanvuli kutoka angani mita 4000 kutoka usawa wa bahari
Watoto wa Halaiki wakionesha umbo la picha za Rais wa Kikwete na Rais Shein na maneno yanayosomeka Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Watoto kutoka Tanzania Bara na Zanziba wakionesha utaalamu wa kucheza ngoma
Kikundi cha Wasanii mbalimbali wakiimba wimbo maalum wa pamoja kuhusu miaka 50 ya Muungano

Picha Reginald Philip.

Makamu wa Rais wa Nigeria awasili nchini kushiriki sherehe za muungano

Ndege iliyo mbeba Makamu wa Rais wa Nigeria Mhe. Mohammed Namadi Sambo ikiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere

Makamu wa Rais wa Nigeria,  Mhe. Mohammed Namad Sambo akishuka katika ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Makamu huyo wa Rais ambaye alimwakilisha Rais wake ni miongoni mwa viongozi wengi watakaoshiriki sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika  na Zanzibar.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akimpokea Makamu wa Rais wa Nigeria Mhe. Mohammed Namad Sambo  baada ya kuwasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Makamu wa Rais wa Nigeria ni miongoni mwa viongozi wengi kutoka duaniani kote watakaoshiriki Maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yatakayofanyika tarehe 26 Aprili, 2014.

Picha na Reginald Kisaka

Friday, April 25, 2014

Naibu Waziri ampokea Waziri Mkuu wa Rwanda atakayeshiriki sherehe za Muungano

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiongozana na Waziri Mkuu wa Rwanda, Mhe. Pierre Habumuremyi mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kilele cha Maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hapo zitakazofanyika tarehe 26 Aprili, 2014.
Mhe. Habumuremyi kwa pamoja na Mhe. Mahadhi wakiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa na moja ya kikundi cha ngoma Uwanjani hapo.
Mhe. Dkt. Maalim akizungumza na Mhe. Habumuremyi huku Balozi wa Rwanda hapa nchini Mhe. Dkt. Benjamin Rugangazi akisikiliza.
Mhe. Habumuremyi na Mhe. Dkt. Maalim wakimsikiliza Balozi Rugangazi wakati akiwaeleza jambo.