Saturday, April 26, 2014

Sherehe za miaka 50 ya Muungano zafana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua  Gwaride Maalum lililoandaliwa kwa ajili ya sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika  na Zanzibar zilizofanyika kwenye Viwanja vya Uhuru jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2014.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Rais wa Uganda Kaguta Yoweri Museveni huku Mfalme Mswati wa Swaziland, Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein wakishuhudia tukio hilo. 
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (aliyenyoosha kidole) akimwonesha kitu Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe wakati wa sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 Kikosi cha Makomando wakionesha mbele ya Mhe. Rais, wageni waalikwa na wananchi mafunzo waliyopitia.
Moja ya zana za  kivita za kisasa zikipitishwa mbele  ya Mhe. Rais Kikwete na wageni waalikwa ikiwa ni moja ya kusherehea miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Ndege za kivita nazo zikipita angani .
Mwanajeshi akitua na mwanvuli kutoka angani mita 4000 kutoka usawa wa bahari
Watoto wa Halaiki wakionesha umbo la picha za Rais wa Kikwete na Rais Shein na maneno yanayosomeka Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Watoto kutoka Tanzania Bara na Zanziba wakionesha utaalamu wa kucheza ngoma
Kikundi cha Wasanii mbalimbali wakiimba wimbo maalum wa pamoja kuhusu miaka 50 ya Muungano

Picha Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.