Friday, April 25, 2014

Waziri Membe ampokea Mfalme Mswati III kwa ajili ya Muungano

Ndege iliyombeba Mfalme Mswati  III wa Swaziland ikiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Mfalme Mswati ni miongoni mwa Viongozi kutoka mataifa mbalimbali duniani watakaoshiriki maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mfalme Mswati III akishuka kwenye Ndege mara baada ya kuwasili nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akiwa pamoja na Mke wake Mama Dorcas Membe (katikati) pamoja na Balozi wetu nchini Msumbiji ambaye anawakilisha pia Swaziland Mhe. Shamim Nyanduga wakishuhudia kuwasili kwa Mfalme Mswati IIi
Waziri Membe akisalimiana na Mfalme Mswati mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius  Nyerere.
Waziri Membe akisalimiana na Mke wa Mfalme Mswati III.
Mfalme Mswati III akisalimiana na viongozi mbalimbali waliokuwepo Uwanjani hapo kwa mapokezi.
Mh. Membe akiongozana  na Mfalme Mswati III mara baada kumpokea
Mama Membe akiongozana na Mama Mswati III


Waziri Membe akizungumza na Mfalme Mswati III walipokuwa wakiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa na kikundi cha matarumbeta (hakipo pichani).
Mfalme Mswati III pamoja na Waziri Membe wakiangalia burudani ya kikundi cha matarumbeta.


Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.