Friday, April 25, 2014

Naibu Spika wa China awasili kwa ajili ya kushiriki sherehe za Muungano


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha National People's Congress cha China na Naibu Spika, Mhe. Chen Changzhi wakimsikiliza Mkalimani wakati wa mazungumzo yao mara baada ya Mhe. Chen kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Mhe. Chen yupo nchini akimwakilisha Rais wa China kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hapo tarehe 26 Aprili, 2014.
Mazungumzo yakiendelea. Kulia kwa Mhe. Chen ni Balozi wa China hapa nchini Mhe. Lu Youqing na kushoto kwa Mhe. Maalim ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.