Sunday, April 20, 2014

Waziri Membe awa Mgeni Rasmi Tamasha la Pasaka

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa na mkewe Mama Dorcas Membe wakiwasili kwenye Uwanja wa Taifa kwa ajili ya kushiriki Tamasha la Pasaka. Mhe. Membe alikuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha hilo lililofanyika siku ya Pasaka tarehe 20 Aprili, 2014.
Mhe. Membe na mkewe wakisalimiana na Waandaaji wa Tamasha la Pasaka akiwemo Kiongozi wao Bw. Alex Msama (wa  kwanza kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Taifa.
Mhe. Membe akiwa ameongozana na Mwandaaji wa Tamasha la Pasaka  Bw. Msama kuingia uwanjani.
Mhe. Membe akisalimia umati wa watu (hawapo pichani)  waliohudhuria Tamasha hilo.
Umati wa Watu waliohudhuria Tamasha la Pasaka.
Mwandaaji wa Tamsha la Pasaka Bw. Msama nae akisalimia watu waliohudhuria
Mama Membe akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Bibi Angela Kairuki ambaye pia alishiriki kwenye Tamasha la Pasaka.
Mmoja wa Waimbaji wa Nyimbo za Injili, Bi. Upendo Nkone akitumbuiza wakati wa Tamasha la Pasaka.
Mhe. Membe akimpongeza Bi. Nkone mara baada ya kutumbuiza.
Mmoja wa Wachungaji waliohudhuria Tamasha la Pasaka akisoma risala maalum kwa Mgeni Rasmi, Mhe. Membe.
Mhe. Membe akitoa hotuba wakati wa Tamasha la Pasaka.
Umati wa watu wakishangilia wakati Mhe. Membe (hayupo pichani) akihutubia.
Balozi Mbelwa Kairuki (katikati), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa naye pia alikuwepo kwenye Tamasha la Pasaka.
Mhe. Membe akiwa na Bw. Richard Kasesera ambaye pia alihudhuria Tamasha la Pasaka.

Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.