Friday, April 25, 2014

Viongozi waanza kuwasili nchini kwa ajili ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim  akimpokea Waziri Mkuu wa Msumbiji,  Mhe. Dr. Alberto Antonio Vaquina mara baada ya kuwasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Waziri Mkuu huyo ambaye ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Eduardo Coloma ni miongoni mwa viongozi wengi kutoka duaniani kote watakaoshiriki Maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yatakayofanyika tarehe 26 Aprili, 2014.
Mhe. Vaquina akiwa na mwenyeji wake Naibu Waziri Mambo ya Nje Dkt. Maalim wakitizama burudani ya ngoma iliokuwa ikitolewa Viwanjani hapo.
Mhe. Dkt. Maalim akizungumza na Dkt. Alberto Antonio Vaquina, Waziri Mkuu wa Msumbiji mara baada ya mgeni huyo kuwasili.

Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.