Thursday, April 10, 2014

Mhe. Membe azungumza na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani

Waziri wa Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ubalozi wa Tanzania mjini Washington D.C, Marekani kwa ajili ya kuzungumza na Wafanayakazi wa Ubalozi huo. Mhe. Membe alikuwa nchini Marekani kwa ajili ya kupokea Tuzo ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi katika Maendeleo ya Bara la Afrika kwa mwaka 2013 kwa niaba ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ametunukiwa Tuzo hiyo.
Mhe. Membe akisaini Kitabu cha Wageni Ubalozini Washington D.C huku Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula akishuhudia.
Mhe. Membe akizungumza na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani (hawapo pichani)
Mhe. Balozi Mulamula (kushoto) akiwa na Mkuu wa Utawala Ubalozini, Bibi. Lily Munanka (katikati) pamoja na Bi. Redemptor Tibaigana, Afisa Mambo ya Nje wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozugumza nao.
Wafanyakazi wengine wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani wakati wa mkutano na Mhe. Membe (hayupo pichani). Kutoka kushoto ni Bw. Suleiman Saleh, Bi. Mindi Kasiga na Bw. Abbas Misana.
Wafanyakazi wengine wa Ubalozi huo akiwemo Dkt. Mkama (kulia), Mama Kijuu (kushoto) wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.