Friday, April 25, 2014

Naibu Waziri ampokea Waziri Mkuu wa Rwanda atakayeshiriki sherehe za Muungano

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiongozana na Waziri Mkuu wa Rwanda, Mhe. Pierre Habumuremyi mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kilele cha Maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hapo zitakazofanyika tarehe 26 Aprili, 2014.
Mhe. Habumuremyi kwa pamoja na Mhe. Mahadhi wakiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa na moja ya kikundi cha ngoma Uwanjani hapo.
Mhe. Dkt. Maalim akizungumza na Mhe. Habumuremyi huku Balozi wa Rwanda hapa nchini Mhe. Dkt. Benjamin Rugangazi akisikiliza.
Mhe. Habumuremyi na Mhe. Dkt. Maalim wakimsikiliza Balozi Rugangazi wakati akiwaeleza jambo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.