Saturday, April 26, 2014

Makamu wa Rais wa Nigeria awasili nchini kushiriki sherehe za muungano

Ndege iliyo mbeba Makamu wa Rais wa Nigeria Mhe. Mohammed Namadi Sambo ikiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere

Makamu wa Rais wa Nigeria,  Mhe. Mohammed Namad Sambo akishuka katika ndege mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Makamu huyo wa Rais ambaye alimwakilisha Rais wake ni miongoni mwa viongozi wengi watakaoshiriki sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika  na Zanzibar.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akimpokea Makamu wa Rais wa Nigeria Mhe. Mohammed Namad Sambo  baada ya kuwasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Makamu wa Rais wa Nigeria ni miongoni mwa viongozi wengi kutoka duaniani kote watakaoshiriki Maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yatakayofanyika tarehe 26 Aprili, 2014.

Picha na Reginald Kisaka

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.