Thursday, April 17, 2014

Waziri Membe akabidhi rasmi Tuzo ya Mhe. Rais Kikwete

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa maelezo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kabla ya kumkabidhi Tuzo ya Heshima ya Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa ziadi katika Maendeleo Barani Afrika kwa mwaka 2013 aliyoipokea kwa niaba ya Mhe. Rais Kikwete tarehe 9 Aprili, 2014 Jijini Washington D.C, Marekani. Heshima hiyo kwa Rais Kikwete ilitolewa na Jarida Maarufu la Kimataifa la African Leadership Magazine Group.
Mhe. Rais Kikwete na Wajumbe wengine waliokuwepo akiwemo Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu wakimsikiliza Mhe. Membe.
Mhe. Membe akimkabidhi rasmi Mhe. Rais Kikwete Tuzo yake. 
Mhe. Rais Kikwete akionesha Tuzo hiyo mara baada ya kuipokea kutoka kwa Mhe. Membe.

Picha na Reginald Phillip.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.