Saturday, April 19, 2014

Waziri Mkuu ahitimisha Maonesho ya miaka 50 ya Muungano

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Mizengo Peter Kayanza Pinda akiongozana na Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb), Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais alipowasili katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufunga rasmi Maonesho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar  rasmi
 19 Aprili, 2014
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda, akihutubia wananchi waliohudhuria sherehe za ufungaji wa Maonesho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Wananchi kutoka  vitongoji mbalimbali vya Jiji la Dar es Salaam wakimsikiliza Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Peter Pinda alipokuwa akihutubia kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mhe. Pinda akiangalia burudani iliyokuwa ikitolewa na moja ya kikundi cha ngoma (hawapo pichani) kilichokuwa kikitumbuiza wakati wa ufungaji wa maonesho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Wengine katika picha ni Mhe.  Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Ummy Mwalimu, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais na Mhe. Raymond Mushi, Mkuu wa Wilaya ya Ilala  ambaye pia alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Kikundi cha Ngoma kikitoa Burudani mbele ya mgeni rasmi Mhe. Pinda (hayupo pichani) wakati wa sherehe za ufungaji wa Maonesho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mkumbwa Ally akipokea Cheti cha Ushiriki wa Wizara kwenye Maonesho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene akizungumza na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Taasisi zake alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wananchi wakiwa katika Banda la maonesho la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.