Wednesday, April 16, 2014

Katibu Mkuu amwakilisha Waziri kumpokea Rais Mstaafu wa Zanzibar alipotembelea Maonesho ya miaka 50 ya Muungano

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akimkaribisha Rais Mstaafu wa Zanzibar, Mhe. Amani Abeid Karume (katikati) kuzungumza na wananchi alipotembelea maonesho ya Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 15 hadi 19 Aprili, 2014. Bw. Haule alikuwa mwenyeji wa Mhe. Karume Viwanjani hapo kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.).

Mhe. Karume akizungumza viwanjani hapo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Mhe. Karume na Bw. Haule wakisikiliza maelezo kutoka kwa Maafisa walipotembelea Banda la maonesho la Benki Kuu ya Tanzania Viwanjani hapo.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.