Thursday, May 8, 2014

Naibu Waziri aongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye uchaguzi Afrika Kusini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya wakielekea kwenye moja ya Vituo vya kupigia kura wakati wa  Uchaguzi Mkuu wa Rais nchini humo uliofanyika tarehe 7 Mei, 2014. Mhe. Dkt. Maalim anaongoza ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi  kutoka Tanzania kama nchi mwanachama wa SADC na pia  mjumbe wa Asasi ya Ulinzi, Siasa na Usalama ya SADC. 


Mhe. Dkt. Maalim akiwa na Waangalizi wengine kwenye moja ya vituo vya kupigia kura mjini Pretoria kabla ya zoezi la upigaji kura kuanza.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waangalizi wa Uchaguzi kwenye Kituo cha Taifa cha Kuratibu Matokeo. Kwa nyuma ni screen zinazoonesha matokeo kutoka sehemu mbalimbali za nchi yanavyoingia.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.