Saturday, May 10, 2014

Mikutano ya Waziri Membe na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki na Wafanyabiashara




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) wa kwanza kulia na ujumbe wake akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki hayupo pichani jijini Istambul siku ya Ijumaa tarehe 09 Mei, 2014. Mhe. Membe aliliomba Shirika hilo liingie ubia na Shirika la Ndege la Tanzania. Ombi ambalo Mkurugenzi Mtendaji aliahidi kulifanyia kazi ambapo wiki ijayo atatuma timu ya wataalamu ili kuongea na timu ya wataalamu ya ATCL kutathmini namna mashiraka hayo yatakavyoweza kushirikiana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki wa katikati pamoja na timu yake ikimsikiliza kwa makini Waziri Membe hayupo pichani.

Ujumbe wa Tanzania na wa Shirika la Ndege la Uturuki wakiendelea na mazungumzo

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki akifanya power point presentation kuhusu utendaji wa shirika lake na matarajio ya kibiashara katika Bara la Afrika na ulimwengu wote kwa ujumla. Alitaja Bara la Afrika kuwa ni bora zaidi kibiashara katika siku zijazo kutokana na ukuaji wa uchumi wa kasi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (kulia) akimkabidhi zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki
Waziri Membe kushoto naye anapokea zawadi yake kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la Uturuki
zawadi kwa Waziri Membe.



 Mkutano wa Waziri Membe na Wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (kati) akiwaeleza wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki (baadhi yao wanaonekana katika picha ya chini) fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini Tanzania. Aliwahamasisha waje kuwekeza Tanzania hususan, katika sekta zitakazoongeza ajira kwa wingi kama vile viwanda vya nguo na kilimo. Wafanyabiashara hao walionesha dhamira ya dhati kuja nchini kuangalia fursa walizotangaziwa.

Baadhi ya Wafanyabiashara wa Uturuki na ujumbe wa Tanzania.

Waziri Membe akibadilishana kadi za mawasiliano na Wafanyabiashara wakubwa wa Uturuki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.