Thursday, May 15, 2014

Waziri Membe afungua Mkutano wa Baraza la Wafanayakazi wa Mambo ya Nje


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.)-katikati) kwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa tatu kutoka kushoto) na viongozi wengine wakiimba wimbo wa "Solidarity" wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Mei, 2014.
Mhe. Membe akitoa hotuba ya ufunguzi wa Baraza la Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambapo alitoa rai kwa Wafanyakazi hao kujituma na kuongeza bidii katika utendaji kazi wao wa kila siku.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Waziri Membe alipofungua kikao cha Baraza hilo.
Katibu Mkuu, Bw. Haule nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo.

Baadhi ya Wajumbe wakimsikiliza Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati akizungumza. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Dushhood Mndeme.
Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Bibi Naomi Zegezege nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo huku Mhe. Membe na Viongozi wengine wakimsikiliza.
Kikao kikiendelea.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Baloiz Vincent Kibwana akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo.
Katibu Mkuu, Bw. Haule, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha na Viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mambo ya Nje.
Waandishi wa Habari nao pia walikuwepo.
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mara baada ya kulifungua.

Picha na Reginald Philip



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.