Friday, May 16, 2014

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Vietnam awasili nchini kwa ziara ya kikazi



Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Vietnam, Mhe. Nguyen Phuong Nga mara baada ya kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Mhe. Nguyen yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tano.




Mhe. Dkt. Maalim na Mhe. Nguyen wakizungumza huku Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Vo Thanh Nam (kushoto), Bw. Nathaniel Kaaya (kulia), Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Asia na Australasia na Bw.Emmanuel Ruangisa, Afisa Mambo ya Nje  wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mhe. Nguyen akimkabidhi zawadi Dkt. Maalim mara baada ya mazungumzo yao.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.