Monday, May 12, 2014

Waziri Membe ashiriki kuuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisaini kwa masikitiko makubwa Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini, Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga kilichotokea kwenye Hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam tarehe 09 mei 2014.
Mhe. Membe akisalimiana na baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini kabla ya kuanza kwa shughuli za kuuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Marehemu Flossie Gomile-Chidyaonga. Shughuli hiyo ilifanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 12 Mei, 2014.
Mhe. Membe akizungumza wakati wa kuuaga mwili wa  aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Marehemu Flossie Gomile-Chidyaonga. Mhe. Membe alimwelezea Hayati Balozi Flossie kama mtu aliyependa amani, mcheshi na msikivu. Alisema Hayati Balozi Flossie alikuwa mstari wa mbele katika suala la mgogoro kati ya Tanzania na Malawi kuhusu Mpaka katika Ziwa Nyasa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. John Haule (wa pili kutoka kulia mstari wa kwanza) akiwa  na Balozi Vincent Kibwana  kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika  pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na  Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati akimwelezea Hayati Balozi Flossie.

Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa kuuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga.
Mhe. Membe akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga. 
Balozi wa Zambia hapa nchini, Mhe. Judith Kangoma Kapijimpanga akishindwa kujizuia wakati wa kuuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga.
Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa, Viongozi kutoka Serikalini, Taasisi Binafsi na watu mbalimbali wakiuaga mwili wa aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga.
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.