Thursday, July 24, 2014

Tanzania na Sri Lanka kuimarisha ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sri Lanka, Mhe. Prof. G.L. Peiris walipokutana mjini Colombo, Sri  Lanka wakati wa ziara ya Mhe. Membe nchini humo hivi karibuni. Wakati wa ziara hiyo  Mhe. Membe kwa niaba ya Serikali ya Tanzania alisaini mikataba mitatu ikiwemo ule wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Sri Lanka, Mkataba wa Ushirikiano katika masuala ya Siasa na Mkataba wa Makubaliano katika Maendeleo na Utafiti wa Kilimo endelevu cha Minazi.
Mhe. Membe na Ujumbe wake (kushoto) wakati wa mazungumzo na Mhe. Peiris na Ujumbe wake (kulia)
Mhe. Membe na Mhe. Peiris wakisaini Mkataba wa kuanzisha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Sri Lanka.
Mhe. Membe na Mhe. Peiris wakibadilishana Mkataba mara baada ya kuusaini.
Mhe. Membe na Waziri wa Kilimo wa Sri Lanka wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Maendeleo na Utafiti wa Kilimo endelevu cha Minazi.
Mhe. Membe na Mhe. Prof. Peiris wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano waliyokubaliana.
Wajumbe kutoka Tanzania na Sri Lanka pamoja na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mhe. Membe na Mhe. Peiris (hawapo pichani)

Monday, July 21, 2014

Waziri Membe ashiriki futari nyumbani kwa Balozi Mdogo Mhe. Omary Mjenga

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akiwa na Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai Mhe. Omary Mjenga wakisubiri muda wa futari mjini Dubai leo. Mhe. Membe alikuwa njiani kuelekea Colombo, Sri Lanka kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola.
Mhe. Membe pamoja na Mhe. Mjenga, wakiwa katika mazungumzo kwenye ukumbi wa mazungumzo (majlis) nyumbani kwa Balozi Mdogo
Waziri Membe akiwa akiwa na Balozi Mdogo Mhe. Omary Mjenga kwenye futari.



Friday, July 18, 2014

PRESS RELEASE


Rt. Hon. Dato' Sri Mohammad NajibTun Abdul Razak

PRESS RELEASE

H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolence message to Rt. Hon. Dato' Sri Mohammad NajibTun Abdul Razak, Prime Minister of Malaysia following the loss of lives due to the crash of a Malaysian airliner on Thursday 17th July 2014. The message reads as follows:

“Rt. Hon Dato' Sri Mohammad Najib Tun Abdul Razak,
The Prime Minister of Malaysia,
Kuala Lumpur.
Malaysia

I have learnt with great shock and sorrow the sad news of the loss of so many lives due to the crash of a Malaysian airliner on its way from Amsterdam to Kuala Lumpur that occurred on Ukrainian territory on Thursday 17th July 2014.

The crash is an immense tragedy not only for the loved ones of those who perished but also for all the people of Malaysia and their friends. As a country, our thoughts and prayers are with the people of Malaysia in this time of grief.

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I offer you our sincere condolences, support and solidarity.

Please accept, Your Excellency the assurances of my highest consideration”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

18th July, 2014

Naibu Katibu Mkuu amuaga Balozi wa Israel nchini

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Gil Haskel, Balozi wa Israel nchini Tanzania ambaye alifika Wizarani kwa lengo la kuaga baada ya kumaliza muda wake. Kwenye mazungumzo yao, Balozi Gamaha ameishukuru Serikali ya Israel kwa ushirikiano mzuri na Serikali ya Tanzania hususan kwenye upande wa kujengea uwezo wa Watanzania kwenye masuala ya Kilimo cha Umwagiliaji. Kwa upande wake Balozi Haskel ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chake. Pia ameahidi kuendeleza ushirikiano huo hata katika wadhifa wake mpya akiwa nchini kwake, ambapo atakua Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Israel.

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati,  Balozi Simba Yahya (kushoto) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (kulia) na Bw. Leonce Bilauri, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia na kunukuu mazungumzo kati ya Naibu Kaibu Mkuu na Balozi wa Israel nchini.

Picha na Reginald Philip

Thursday, July 17, 2014

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Hungary nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho za Mhe. Sander Kocsis, Balozi wa Hungary nchini Tanzania mwenye makazi Nairobi, Kenya. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam hivi karibuni.
Balozi Kocsis akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Balozi Kocsis akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara baada ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais.
Balozi Kocsis akisalimiana na Balozi Joseph Sokoine, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Kocsis.

Mhe. Rais katika picha ya pamoja na Balozi Kocsis, Waziri Membe na Mhe. Mark Mwandosya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum.
Balozi Kocsis akisikiliza wimbo wa taifa lake uliopigwa na bendi ya polisi (haipo pichani) kwa heshima yake. Wengine katika picha ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohhamed Maharage Juma (kulia) na Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo (kushoto)
ASP Kulwa akiongoza Bendi ya Polisi wakati wa mapokezi ya Balozi Kocsis (hayupo pichani)

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Shelisheli nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hatiza Utambulisho za Mhe. Claude Morel, Balozi wa Shelisheli hapa nchini mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.
Balozi Morel akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Morel, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) huku Prof. Mark Mwandosya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum akishuhudia.
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Morel.
Mhe. Balozi Morel (katikati) akisikiliza wimbo wa taifa lake mara baada ya kuwasili Ikulu. Wengine katika picha ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohamed Maharage Juma (Kulia) naBw. Shaaban Gurumo, Mnikulu. 
Bendi ya Polisi ikiongozwa na ASP Kulwa wakiwa kazini

Wednesday, July 16, 2014

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa New Zealand hapa nchini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Richard Stuart Mann, Balozi wa New Zealand hapa nchini mwenye makazi yake Afrika Kusini. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.

Balozi Mann akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara baada ya Balozi huyo kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Kikwete, wakwanza kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi maalum Mhe. Prof. Mark J. Mwandosya (Mb.)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Richard Stuart Mann
Balozi Richard Stuart Mann akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Balozi Mann akisikiliza Wimbo wa Taifa lake ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na wakwanza kushoto ni Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo


Picha na Reginald Philip



Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Ujerumani nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Egon Kochanke, Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.
Balozi Kochanke akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Egon Kochanke
Picha ya pamoja
Balozi Kochanke akisikiliza Wimbo wa Taifa lake ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na kushoto ni Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo

Picha na Reginald Philip

Membe awa mgeni rasmi siku ya Taifa ya Ufaransa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza katika hafla ya kusheherekea siku ya Taifa la Ufaransa. Halfa iliyofanyikia katika makazi ya Balozi wa taifa hilo nchini, Mhe. Marcel Escure Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kulia ni Mkuu wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Juma Alfani Mpango. 
Mhe. Membe akizungumza wakati wa hafla hiyo huku wageni waalikwa wakimsikiliza.


Picha na Reginald Philip

Waziri Membe azungumza na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha St. Thomas cha Marekani

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na kiongozi wa wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha St. Thomas, Fr. Jean-Piere Bongilo kilichopo  Minessota nchini Marekani waliofika Wizarani kumsalimia. Chuo cha St. Thomas kilimtunuku Shahada ya Uzamivu wa Heshima, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2006.
Baadhi ya Wanafunzi hao wakimsikiliza Mhe. Membe alipozungumza nao.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatifa, Balozi Joseph Sokoine (wa kwanza kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kushoto) na baadhi ya wanafunzi hao.
Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo na wanafunzi hao.
Picha na Reginald Philip


Monday, July 14, 2014

Waziri Membe azungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (Mb.)  akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini kuhusu masuala mbalimbali ya nchi ikiwa ni pamoja na  nia ya kikundi cha uasi cha FDLR ya kuweka silaha chini na ziara ya Mabalozi na Wawakilishi hao Butiama. Wengine katika picha ni  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.),  kulia kwa Waziri Membe,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje Bw. John Haule (wa kwanza kulia),   Mkuu wa Mabalozi na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) , Mhe.  Juma Alfani Mpango (wa pili kulia) na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha (wa kwanza kushoto) . Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Mabalozi wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini wakimsikiliza Mhe. Membe.
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa katika kikao kati ya Mabalozi wa Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini.
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  na Balozi wa Sudan hapa nchini (kulia) wakifuatilia maelezo ya Mhe. Membe (hayupo pichani)
Mabalozi, Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini pamoja na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)


Waziri Membe akisalimiana na Mwakilishi wa Papa Bennedict XVI hapa nchini, Balozi Francisco Montecillo Padilla mara baada ya kumaliza kikao.
Mhe. Membe akisalimiana na Balozi wa Zambia hapa nchini, Mhe. Judith Kangoma Kapijimpanga.
Mhe. Membe akitoa taarifa kwa  Waandishi wa Habari kuhusu mazungumzo kati yake na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakiwa kazini
Mhe. Membe akiendelea kutoa taarifa kwa Waandishi wa Habari
Meza kuu wakimsikiliza Mhe. Membe (Picha na Reginald Philip)
--------------------------------------------------------------------

Hon. Membe urges international support to dissolve FDLR

The Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard Membe, has urged the international community to support implementation of the Angola Declaration on the dissolution of the Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR).

The declaration to dissolve the largest remaining negative forces in the Democratic Republic of Congo (DRC) was adopted by a SADC/Great Lakes Region Ministerial meeting held in Luanda, Angola on July 2, 2014. Tanzania is a member of the SADC Organ Troika on Politics, Defence and Security Cooperation.

Hon. Membe told diplomats accredited to Tanzania in Dar es Salaam today, that the Angola declaration was prompted by a letter to SADC by the FDLR, offering voluntary surrender.

“As we speak, 350 soldiers of FDLR have surrendered and are cantoned in a camp near Kinshasa,” the Minister told the foreign diplomats, adding that SADC found it logical and legally correct to accept the FDLR offer of surrender.

He said the process to dissolve the negative forces would involve five stages: Disarming the soldiers; demobilizing the group; repatriating the soldiers to Rwanda, reintegrating those meriting into the national army and resettling the rest.

This process required the participation of the United Nations, DRC government, Rwanda government, which should accept repatriation, reintegration and resettlement of  FDLR troops; SADC and the international community, which would monitor implementation.

“The monitoring teams should have truly international character, and that is where your assistance is needed,” Hon. Membe told the diplomats.

He said the FDLR had been give six months from this month to comply with the dissolution plan failing which the UN combat force in DRC would be used to disable the negative force.

Hon. Membe said the acceptance of the surrender notice would not exonerate criminal elements among FDLR ranks from punishment. “If any members of the group are found to have committed crime they will be prosecuted,” he explained.

Meanwhile, Hon. Membe has expressed Tanzania’s disapproval of ongoing killing of civilians by Israeli air strikes in Gaza, which have so far claimed over 170 lives.

Addressing a press conference after the meeting with diplomats, the Minister called on Israel and Hamas to ceasefire immediately, adding that The United Nations Security Council should step in to restore harmony in the Middle East.

In another development, Hon. Membe announced that his Ministry was organizing a “World in Butiama” expedition in October, this year, which would take foreign diplomats accredited to Tanzania to the burial site of The Father of the Nation, Mwalimu Nyerere, to pay homage.


-Ends-


PRESS RELEASE

 H.E. Francois Hollande

PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency Francois Hollande, President of France on the occasion his country’s National Day on 14th July, 2014.

The message reads as follows;

        “His Excellency Francois Hollande,
President of France,
Paris,

FRANCE.


Your Excellency,

On behalf of the government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I wish to convey my sincere congratulations to you and through you to the Government and people of France on the occasion of your country’s National Day on 14th July, 2014.

We in Tanzania cherish the close ties of friendship, cooperation and partnership that so happily exist between our two countries. Over the years these links have increasingly strengthened to the benefit of our peoples. Together we have built bridges between our two countries in every conceivable field from education, tourism, water, sanitation, governance, regional cooperation, commerce and trade.

Please accept, your Excellency, my best wishes for your personal good health and peace and prosperity for the people of France”.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam
14th July, 2014