Thursday, January 8, 2015

Wadau wajadili sera ya Taifa ya Mtangamano ya Afrika Mashariki


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akifungua kikao cha wadau cha kujadili Sera ya Taifa ya Mtangamano wa Afrika Mashariki, katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba yahaya akiwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Said Seif Mzee  wakifuatilia hotuba
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Irene Kasyanju pamoja na Mkuu wa Kitengo cha TEHEMA Bwa. Isack Kalumuna wakisikiliza Hotuba ya ufunguzi. 
Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje Bw. James Lugaganya akitoa mada kwa wadau kuhusu mambo muhimu yaliyozingatiwa katika Sera ya Taifa ya Mtangamano ya Afrika Mashariki

Wadau wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Bw. Lugaganya
Sehemu nyingine wadau
Balozi Mstaafu Vincenti Kibwana akichangia jambo katika kikao hicho
Mdau, Bi. Grace Naburi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi naye akitoa mchango wake kuhusi sera hiyo


Mdau, Bw. Justin Moshi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria
Mdau, Bi. Mindi Kasiga kutoka Wizara ya Mambo ya Nje nae akichangia mada
Wadau mbali mbali wakiwa katika kikao.
Kikao kikiendelea





Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule akiwa katika Picha ya pamoja na wadau.


Picha na Reginald Philip 

Wednesday, January 7, 2015

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Balozi wa Syria

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Maadhi Juma Maalimu (Mb) akimkaribisha Balozi wa Syria Nchini Mhe. Abdulmonem Annan, alipokuja kumtembelea na kumweleza kuhusu hali ya kisiasa inavyoendelea nchini Syria 
Balozi Abdulmonem Annan akizungumza na Mhe. Maadhi Juma Maalim
Mazungumzo yakiendelea.


Picha na Reginald Philip

Mada kuhusu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia na athari zake kwa nchi yawasilishwa kwa maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje

Bw. Allan William mtaalamu wa sekta za kibenki nchini, akizungumza katika mhadhara na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa juu ya Mwenendo wa bei za mafuta duniani  na athari zake kwa nchi yetu, mhadhara huo umefanyika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa JNICC uliopo jijini Dar es Salaam mapema leo Asubuhi.
Balozi Simba Yahaya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati (wa kwanza kulia), Balozi Mbelwa Kairuki (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Austrasia na Bw. Togolani Mavura kwa pamoja wakimsikiliza kwa makini Bw. Allan William.
Maafisa wa Wizara wakisikiliza kwa makini 
Balozi Simba Akichangia mada katika muadhara huo.
Bw. Adam Elinawinga kutoka kampuni ya PUMA naye akiendelea kuelezea mwendendo mzima wa bei za mafuta duniani na athari zake kwa nchi yetu. 
Msaidizi wa Rais (hotuba) Bw. Togolani Mavura akichangia mada katika muhadhara huo
Maafisa wa Wizara.
Mhadhara ukiendelea.
Picha na Reginald Philip


Monday, January 5, 2015

MEMBE APONGEZA ANGLIKANA KUPINGA USHOGA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamillius Membe akizindua sherehe ya miaka 50 ya Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es salaam, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano, jijini Dar es salaam jana Jumapili, Januari 4, 2015, akishuhudiwa na  Dk. Valentine Mokiwa, Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam.
Waziri Membe akizungumza katika sherehe hiyo
Wachungaji wakimsikiliza Mheshimiwa Membe kwa makini wakati akiongea.
Masista nao wakifuatilia  
Askofu Mokiwa akitoa mahubiri katika ibada ya uzinduzi wa sherehe ya miaka 50 ya Diyosisi ya Dar es Salaam. .
Waziri Membe akisikiliza mahubiri yaliyokuwa yakitolewa na Askofu Valentino


Mahubiri yakiendelea.
Mwimbishaji kwaya akiwaimbisha nyimbo wanakwaya waliovalia majoho ya rangi ya blue na nyeupe.
Mcheza kinanda akisindikiza kwaya ya kanisa






Waziri Membe akikaribishwa na Askofu Mokiwa kwaajili ya utoaji wa vitabu vya kuchangishia fedha kwa ajili ya miradi ya Dayosisi
Waziri Membe aliaanza kumkabidhi kitabu cha Harambee Askofu Mokiwa
Ibada ikiendelea.

Picha na Reginald Philip

======================================

MEMBE APONGEZA ANGLIKANA KUPINGA USHOGA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, amelipongeza Kanisa la Anglikana Tanzania kwa kusimama kidete kupinga ndoa za jinsia moja, hata pale makanisa mengine ya Anglikana duniani yalipounga mkono suala hilo.
Akizindua sherehe za Miaka Hamsini tangu kuanzishwa kwa Dayosisi ya Dar es Salaam ya Kanisa hilo jana, Mhe. Membe alisema msimamo huo wa Kanisa na Watanzania uliipa serikali nguvu kukataa shinikizom kutoka nchi za Magharibi kwamba iidhinishe ushoga hapa nchini.
"Mlinitia nguvu sana pale niliposimama kidete kuwaambia rafiki zetu wa nje kuwa katika hilo la ndoa za jinsia moja, Tanzania tunaomba tukubaliane kutokukubaliana," alisema Mhe. Waziri, wakati wa uzinduzi huo uliofanyikia kwenye kanisa la Mtakatifu Albano, jijini Dar es Salaam. Sherehe za Miaka 50 ya Dayosisi ya Dar es Salaam zitafikia kilele Julai, mwaka huu.
Mhe. Membe alisema serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa la Anglikana na madhehebu mengine ya dini kuboresha maisha ya Watanzania. "Naomba muendelee kushirikiana na serikali katika kutoa huduma kwa wananchi," aliwaambia waumini na waalikwa wengine waliohudhuria misa maalum ya uzinduzi iliyoongozwa na Askofu Valentine Mokiwa.
Aliwataka viongozi wa dini kuombea nchi umoja na  amani, na kuhimiza waumini wao kushiriki kikamilifu katika matukio mawili muhimu yanayolikabili taifa mwaka huu -- Kura ya maoni ya Katiba inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge.
Uchaguzi wa Rais ni muhimu kwa sababu "Rais wa Awamu ya Tano atategemewa kuendeleza mema ya Awamu ya Nne na awamu zilizopita, na kutoa majawabu kwa changamoto za sasa na zijazo na kutusogeza karibu zaidi na Tanzania njema tunayoitamani, Tanzania yenye neema tele. Hatuko mbali na nchi yetu hiyo ya ahadi," alisema.

Mhe. Membe alishambulia rushwa na ifisadi kuwa ndivyo vinavyodidimiza nchi na kuongeza umasikini kwa wananchi licha ya Tanzania kuwa na rasilimali lukuki. "Tuchague viongozi waadilifu, wazalendo, wachapa kazi, wasio na uchu wa madaraka kwa ajili ya kujinufaisha wao binafsi na marafiki zao," alisema.
Alitaka vijana waandaliwe vyema kushiriki ujenzi na ulinzi wa taifa kwani ndio warithi. "Tukiwaandaa vyema,mustakabali wa taifa letu na watu wake utakuwa kwenye mikono salama. Tukishindwa leo, tutalia na kusaga meno kesho," alionya.

Monday, December 29, 2014

PRESS RELEASE

Hon. Dato' Sri Mohd Najib bin Tun Abdul Razak.  Malaysian Prime Minister

President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete has sent a condolence message to the Prime Minister of Malaysia,  Honourable Dato’ Sri Mohd Najib bin Tun Abdul Razak, following the worst flooding in more than a decade in Northeastern Malaysia that claimed at least 7 lives and forced nearly 160,000 people from their homes on 27th December, 2014. 


The message reads as follows:

“The Honourable Dato' Sri Mohd Najib bin Tun Abdul Razak,  
Prime Minister of Federal Government of Malaysia,
Putrajaya, MALAYSIA.

Honourable Prime Minister,

I have learnt with deep sorrow the worst flooding in Northeastern Malaysia in more than a decade which occurred on the 27th December, 2014 leading to the loss of lives of at least 7 people and forced nearly 160,000 from their homes.

On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I wish to convey to you, Honourable Prime Minister, and through you, to the Government and People of Malaysia, especially the families of the bereaved, our heartfelt condolence and deep sympathies.

At this moment of intense grief, the People of Tanzania wishes the victims of this calamity a full and speedy recovery amid the worst deluge in living memory of many Malaysians. Our thoughts and prayers are with the Malaysian people during this very difficult time of bereavement.

Please accept, Honourable Prime Minister, the assurances of my highest consideration.


Issued by: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM
                                                                      

29TH DECEMBER, 2014

Wednesday, December 24, 2014

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani awasilisha Hati za Utambulisho kwa Papa Francis

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani,  Mhe. Philip Sang'ka Marmo, amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Baba Mtakatifu Francis, Vatican-Roma, Italia. Balozi Marmo anawakilisha Ujerumani na ndiye anayemwakilisha Mheshimiwa Rais kwa Baba Mtakatifu (Holy See). Kwa utaratibu Mabalozi waliopo Italia hawaruhusiwi kuwakilisha nchi zao kwa Baba Mtakatifu yaani Holy See. Nchi nyingine ambazo Mhe. Balozi Marmo anawakilisha ni Austria, Bulgaria, Jamhuri ya Czech, Hungaria,Ujerumani, Poland, Slovakia, Romania na Switzerland.
Balozi Marmo akiwa katika picha ya pamoja na Baba Mtakatifu Francis
Baba Mtakatifu Francis akimsalimia Mtoto wa Mmoja wa Maafisa walioambatana na Balozi Marmo
Baba Mtakatifu Francis akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi waliowasilisha Hati zao za utambulisho, kulia kwa Baba Mtakatifu ni Balozi Philip Marmo na kushoto kwa Baba Mtakatifu ni Mke wa Balozi Marmo.

Monday, December 22, 2014

Rais Zuma akutana kwa mazungumzo na Rais Kikwete Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akimkaribisha Ikulu Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma alipofika kwa ajili ya mazungumzo rasmi. Mhe. Zuma amehitimisha ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 22 Desemba, 2014 baada ya kufanya mazungumzo na Rais Kikwete.
Rais Kikwete akimkaribisha  Rais Zuma kwenye chumba cha mazungumzo.
Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Rais Zuma wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa pili kulia)  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Maite Nkoana-Mashabane (wa kwanza kushoto).



Konseli Mkuu wa Tanzania Dubai, aagana na maafisa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Konseli Mkuu wa Tanzania Dubai Omar Mjenga (watatu toka kushoto) katika picha ya pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walipotembelea ofisini kwake kumuaga. Maafisa hawa ni kati ya timu imara iliyofanikisha ziara ya kikazi ya Mh. Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda nchi za Falme za Kiarabu.

Rais Zuma awasili nchini kwa ziara ya kikazi

Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma akiteremka kwenye ndege mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam usiku wa tarehe 21 Desemba, 2014. Mhe. Zuma yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo pamoja na mambo mengine atafanya mazungumzo rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete tarehe 22 Desemba, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akiwa tayari kumpokea Mhe. Zuma alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi.
Mhe. Zuma akipokelewa na Mhe. Dkt. Bilal mara baada ya kuwasili nchini. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Itifaki, Balozi Juma Maharage
Mhe. Zuma akisalimiana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye alikuwepo uwanjani hapo kwa mapokezi
Mhe. Rais Zuma akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala wakati wa  mapokezi yake.
Rais Zuma kwa pamoja na Dkt. Bilal wakifurahia burudani ya ngoma iliyokuwa ikitolewa na moja vikundi vilivyokuwepo Uwanjani hapo wakati wa mapokezi.

Saturday, December 20, 2014

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma anatarajiwa kuwasili nchini usiku wa tarehe 21 Desemba, 2014 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Mhe. Zuma atapokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Zuma atakutana kwa mazungumzo rasmi na Mhe. Rais Kikwete tarehe 22 Desemba, 2014 kabla ya kuondoka nchini na kurejea nchini kwake.


IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM.


20 DESEMBA, 2014

Thursday, December 18, 2014

Press Release

Hon. Tony Abbott, Australian Prime Minister

PRESS RELEASE

President of the United Republic of Tanzania, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete has sent a condolence message to the Prime Minister of the Australian Government, Honourable Tony Abbott (MP) following the Sydney café siege which occurred on the 16th December, 2014 and claimed the lives of two people.

The message reads as follows:

“The Honourable,
 Tony Abbott (MP)
 Prime Minister of Australia,
 Canberra, AUSTRALIA.

Honourable Prime Minister,

I am deeply saddened by the Sydney cafe siege on the 16th December 2014 that claimed the lives of 2 people. The attack was indeed received with great shock in my country particularly at this time when the world is seen to be working together to end the scourge.

As the people of Australia continue to grieve for the loss of their loved ones, the Government and the people of the United Republic of Tanzania reiterates its continued support to the Australian Government on the fight against terrorism and wish the bereft families a full and fast recovery from the tumor.

Please accept, Honourable Prime Minister the assurances of my highest consideration”.

Issued by: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

18TH DECEMBER, 2014