Friday, November 4, 2016

MTANZANIA ANG′ARA UMOJA WA MATAIFA



Jana, tarehe 03 Novemba, 2016, Nchi Wanachama wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa zimemchagua kwa mara ya pili mtanzania Prof. Chris Maina Peter, Mhadhiri wa sheria katika Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuwa Mjumbe wa Kamisheni ya Sheria za Kimataifa ya Umoja wa Mataifa (the International Law Commission (ILC) yenye jumla ya Wajumbe 34.



Kwa mara ya kwanza Prof. Peter alichaguliwa kwa mara ya kwanza Novemba 2011, kuwa Mjumbe kwenye Kamati hiyo kwa kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia 2012-2016, hivyo ushindi huo utamfanya kuwa Mjumbe kwenye Kamati hiyo kwa kipindi kingine cha miaka 5 kuanzia 2017-2021. Kwa upande wa Afrika, uchaguzi huo ulijumuisha wagombea 16 kuwania nafasi nane za Bara hilo, ambapo wagombea kutoka nchi za Algeria, Misri, Kenya, Moroko, Afrika Kusini na Tanzania waliibuka kidedea kwenye uchaguzi huo.



Kamisheni ya Sheria za Kimataifa ya Umoja wa Mataifa (Iternationa Law Commission (ILC) ilianzishwa mwaka 1948 kwa madhumuni ya kufanya tafiti, kuendeleza na kutunga sheria za Kimataifa (promotion/research, development and codification of international law). Sambamba na majukumu hayo, ILC inao wajibu wa kuushauri Umoja wa Mataifa kuhusu masulaa yote yanayohusu sheria za kimataifa.



Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kumpongeza Prof. Chris Maina Peter kwa ushindi huo ambao si kwamba umemjengea heshima kubwa yeye peke yake bali Tanzania kwa ujumla. Wizara itaendelea kutoa msaada na ushauri kwa Prof. Peter na Watanzania wengine wenye nafasi kama hizo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa na hivyo kuongeza na kuimarisha nguvu na ushawishi wa Tanzania katika Mahusiano ya Kimataifa na Diplomasia kwa ujumla. Aidha, Wizara inapenda kuwakumbusha Watanzania wote wenye sifa za kitaaluma kuchangamkia nafasi mbalimbali za ajira zinazotolewa na Umoja wa Mataifa na Jumuiya nyingine za Kikanda pamoja na kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za kiutendaji zinazojitokeza.





Thursday, November 3, 2016

WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA BALOZI WA UMOJA WA FALME ZA KIARABU NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Falme za kiarabu nchini Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Al Suweid katika mazungumzo yao balozi Al Suwied alimweleza Mhe. Waziri juu ya maandalizi ya Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) baina ya Tanzania na UAE ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 19 na 20, Dicemba, 2016 huko Abu Dhabi, UAE.
Wa kwanza kulia ni Katibu wa Waziri Bw. Gerald Mbwafu pamoja na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Hangson Mgaka, nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati Waziri Mahiga na Balozi Al Suweid (Hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea




********************************************


Tarehe 04 Novemba, 2016, Mhe. Dkt. Augustine P Mahiga (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Al Suweid, Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini. Balozi huyo alikuja kuzungumzia maandalizi ya Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) baina ya Tanzania na UAE ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 19 na 20, Disemba, 2016 huko Abu Dhabi, UAE. 

Sambamba na Mkutano wa JPC, Mheshimiwa Waziri na Balozi walizungumzia pia kuhusu ombi la UAE la kufanyika Kongamano la Biashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na UAE ambalo UAE imependekeza lifanyike wakati wa mkutano wa JPC huko Abu Dhabi, UAE.


Katika mkutano huo wa JPC maeneo ya ushirkiano ambayo yatazungumziwa na kukubaliwa ni pamoja na sekta ya Uchumi, Miundombinu (Bandari, Viwanja vya Ndege pamoja na Reli), Biashara, Uwekezaji, Viwanda, Kilimo, Afya, Utalii pamoja na Nishati ya Mafuta na Gesi. 

Aidha, viongozi hawa walizungumzia pia mikataba mbalimbali ambayo itasainiwa wakati wa mkutano huo wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano. Mheshimiwa Balozi alisisitiza kuwa Tanzania itumie fursa hii adhimu kwa kujiandaa kikamilifu katika kukuza ushirikiano wa kiuchumi na UAE. 

Kwa upande Mheshimiwa Waziri Mahiga alishukuru kupokea taarifa hiyo na kuahidi kufuatilia kwa karibu ili kuona Mkutano huo wa JPC unafanyika na kufanikiwa kwa manufaa za nchi zote mbili.

Waziri Mahiga afungua Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na Usalama ya SADC


Waziri wa Mambo ya Nje na Uashirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC uliofanyika katika Ukumbi Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine katika Mkutano huo wanatarajia kujadilia hali ya kisiasa katika Nchi za Deokrasia ya Congo na Lesotho

Sehemu ya baadhi ya waandishi wa habari na wajumbe wa mkutano wakimsiliza Mhe. Waziri Dkt. Mahiga wakati akitoa hutuba ya ufunguzi.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt. Stregomena Tax akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda  Balozi Innocent Shiyo (kushoto) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC. Mezakuu  ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, (katikati) Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Aziz Mlima (kulia) na Katibu Mkuu SADC Dkt. Stregomena Tax (kushoto)

Mkurugenzi wa ushirikiano wa Kimataifa akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy (kushoto) akifafanua jambo wakati akifanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa nchini Canada Mhe. Sarah Fountain Smith (kushoto) alipotembelea Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo wamezungumzia masuala mbalimbali ya kimaendeleo ya jamii na uchumi ambayo yanalenga kudumisha na kukuza uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akimsikiliza Naibu Waziri wa Canada Mhe.Sarah Fountain Smith wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam

Balozi Celestine Mushy akimkabidhi kitabu Mhe. Sarah Fountain Smith
Tokea kushoto; Balozi wa Canada nchini, Mhe.Ian Myles, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Sarah Fountain Smith, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, maafisa kutoka Wizarani Bi. Ngusekela Nyerere na Bi. Lilian Kimaro  wakiwa katika picha ya pamoja.



2017 SADC SECONDARY SCHOOL ESSAY COMPETITION



Joint Communique Between Tanzania and Morocco

                        


                           
JOINT COMMUNIQUE BETWEEN THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND THE KINGDOM OF MOROCCO ISSUED AT THE CONCLUSION
OF THE STATE VISIT TO THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
BY HIS MAJESTY MOHAMMED VI, KING OF MOROCCO

1.             At the invitation of His Excellency Dr. John Pombe Joseph Magufuli, President of the United Republic of Tanzania, His Majesty Mohammed VI, King of Morocco paid a State Visit to the United Republic of Tanzania from 23rd to 25th October, 2016.  During visit, His Majesty Mohammed VI was accompanied by a high level delegation, including Ministers, Senior Officials of the Government of the Kingdom of Morocco, as well as members of the Moroccan business community.
2.             In a cordial and friendly atmosphere, the two countries have decided to work together and coordinate their respective efforts to address the challenges that Africa faces in terms of development, stability and security.
3.             President Magufuli commended the leadership of His Majesty King Mohammed VI and paid tribute to His role in promoting peace, stability and development in Africa. He recognized that the South-South cooperation advocated by His Majesty the King Mohammed VI – based on pragmatism, efficiency and public-private partnership is at the core of development cooperation in Africa.
4.             President Magufuli also paid tribute to the leading role that Morocco has been playing in promoting economic growth and sustainable development in various international fora and commended Morocco’s decision to host COP.22 meeting from 7 - 18 November 2016, in Marrakech.
5.             On bilateral issues, the two Heads of State commended the friendly relations between the two countries and committed to work together with a view to further strengthening    the bilateral relations between the two brotherly countries. They reiterated their readiness to establish an Embassy of the Kingdom of Morocco in Tanzania and a Consulate General of the United Republic of Tanzania in Morocco.
6.             In this context, they further vowed to enhance these ties of friendship of cooperation in various fields, including tourism, agriculture, railway transport, and trade. They also pledged to continue exploring new areas of cooperation, such as in economic, scientific, technical and cultural domains, as well as security cooperation and fight against terrorism and radicalism, for the mutual benefit of the two countries and peoples.
7.             To that end, they commended Tanzania-Morocco Trade and Investment Forum that was held on 22nd October 2016, which offered an opportunity for business leaders from the two countries to discuss ways and means to promote two-way trade and set up a win-win economic partnership.
8.             They also witnessed the signing of a number of Agreements and Memoranda of Understanding between both countries in the public and private sectors, covering cooperation on a wide range of areas, including political consultations, agriculture, fisheries, energy, logistics, air services, culture, science and technology, tourism, air services and finance.
9.             In order to realize the desired gains for their two peoples, the two Heads of State directed their Ministers and Senior Officials to work determinedly to implement the signed agreements between Morocco and Tanzania. It is in this spirit that His Excellency President Magufuli declared that henceforth the referral visa requirement for citizens of Morocco coming to Tanzania has been lifted.
10.         On international issues, the two Heads of State discussed the decision of Morocco to rejoin the African Union. In this respect, H.E. Dr. John Pombe Joseph Magufuli expressed Tanzania’s support to Morocco's decision to integrate and find its rightful place in the African Union. He further expressed his readiness to support the admission of Morocco to the Pan – African Institutional family as early as the next Summit.  The two Heads of State expressed their hope that the return of Morocco to the African Union would pave the way to address the longstanding political and diplomatic issues of concern to Morocco.
11.         Regarding the Sahara issue, H.E. Dr. John Pombe Joseph Magufuli expressed the support of Tanzania to the efforts by the United Nations to reach a just, lasting and mutually agreed solution. In the spirit of reconciliation and search for a lasting solution, Tanzania understands the established position of Morocco, welcomes its serious and credible Moroccan efforts and is ready to contribute towards implementation of the relevant resolutions of the United Nations on this issue.
12.         The two Heads of States share the same ambitious vision for Africa masters of its own destiny, in charge of its own development and committed to the path of stability. They underscored, in this regard, the need to strengthen South-South and triangular cooperation, and to promote a continuous and sustainable development, based on the valuation of own African resources and skills.
13.         During the visit, His Majesty Mohamed VI also unveiled the plaque for the construction of a Mosque to be erected with the gracious contribution of His Majesty the King of Morocco at the BAKWATA Headquarters in Dar es Salaam.
14.         At the conclusion of the Official Visit, His Excellency President Dr. John Pombe Joseph Magufuli expressed his profound gratitude and appreciation to His Majesty Mohammed VI for honoring his invitation and for the fruitful discussions they held. On his part, His Majesty Mohammed VI expressed his profound gratitude and appreciation to His Excellency President Dr. John Pombe Joseph Magufuli, the Government and People of the United Republic of Tanzania for the invitation extended to him as well as the warm reception and hospitality accorded to him and his delegation during the entire duration of his visit. Finally, the two Heads of State underscored their firm desire and commitment of their respective Governments to strengthen the ties of friendship and cooperation between the two countries.

           Done at Dar es Salaam, on 26th October, 2016

Wednesday, November 2, 2016

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje afungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Troika ya SADC

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Kikao cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC Troika), Balozi Dkt. Aziz Mlima akifungua rasmi Kikao cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi kutoka Asasi hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupitia agenda mbalimbali zitakazowasilishwa na kujadiliwa kwenye Kikao cha Mawaziri kitakachofanyika tarehe 03 Novemba, 2016 katika Ukumbi huo. Asasi ya SADC inaundwa na nchi tatu ambazo ni Tanzania (Mwenyekiti),  Angola (Makamu Mwenyekiti) na Msumbiji (Mwenyekiti aliyemaliza). Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika, Mhe. Dkt. Stergomena Tax.
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu. Kulia ni Balozi Mlima.
Sehemu ya Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi kutoka Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa kikao. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi HassanYahya Simba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Bw. Job Masima na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Innocent Shiyo.
Sehemu ya Ujumbe wa Msumbiji wakifuatilia ufunguzi wa mkutano huo


Sehemu ya ujumbe kutoka Angola wakati wa ufunguzi wa kikao cha Makatibu Wakuu
Sekretarieti ya SADC
Sehemu nyingine ya ujumbe wa Tanzania wakati wa kikao hicho cha Makatibu Wakuu

Balozi Msechu azindua zoezi la kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi

Balozi wa Tanzania katika Nchi za Nordic na Baltic mwenye makazi yake Sweden,  Mhe. Dora Msechu wa pili kutoka kulia akikata utepe kuashiria uzinduzi wa zoezi la kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera lilifanyika Stockholm, Sweden. Hafla hiyo iliandaliwa na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Sweden kwa lengo la kuhamasisha Watanzania waishio Sweden kuchangia Wahanga wa Maafa ya tetemeko la ardhi Mkoani Kagera. Zoezi hili maalum la kuchangia maafa linaendelea mpaka tarehe 4 Novemba, 2016 na michango itakayopatikana itakabidhiwa kwa Mhe. Balozi Dora Msechu

Mhe. Balozi Dora Msechu akizungumza wakati wa hafla hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania katika Mji wa Malmo ambaye aliwasilisha salaam za watanzania waishio Malmo

Sehemu ya wadau walioshiriki hafla hiyo

Mwanadiaspora Mbarouk Rashidi akikabidhi vifaa kwa Mhe.Balozi Dora Msechu

Kocha Mkuu wa Kilimanjaro FC, Bw. Humphrey Kalanje akizungumza katika hafla hiyo

Tuesday, November 1, 2016

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kutoka Liberia

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akizungumza na Mkurugenzi wa Mipango, Maendeleo na Uratibu kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Liberia, Bw. Theophilus Addey. Katika mazungumzo yao yalijikita katika kuelezea namna Serikali ya Tanzania inavyofanya kazi na Umoja wa Mataifa kupitia Mfumo wa One United Nations (One UN). Balozi Mushy alimweleza Bw. Addey kuwa Tanzania imekuwa nchi ya mfano wa kuigwa kutokana na mafanikio  makubwa yaliyofikiwa katika utekelezaji wa mfumo huo tangu kuanzishwa kwake hapa nchini mwaka 2007. Bw. Addey ameambatana na ujumbe wa pamoja kutoa Serikali ya Liberia na Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini humo.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Bw. Addey wafuatilia mazungumzo.
Sehemu ya Maafisa wa Mambo ya Nje nao wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mushy na Bw. Addey (hawapo pichani)
Sehemu nyingine ya Maafisa Mambo ya Nje.
Balozi Celestine Mushy akimwelezea Bw. Theophilus Addey kitabu kinachoelezea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini
Balozi Mushy akiwa katia picha ya pamoja na ujumbe wa pamoja kati ya Serikali ya Liberia na Ofisi ya Umoja wa Mataifa. 

NI MUHIMU ICC NA AFRIKA KUZUNGUMZA –TANZANIA

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipopokea na kujadili Ripoti ya Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ( ICC) hapo jumatatu. Katika kuchangia Ripoti hiyo, Tanzania imesisitiza haja na umuhimu kwa ICC kukaa na kuzungumza na Nchi za Afrika ili kutafuta suluhu ya misuguano baina ya pande hizo mbili.

 ****************************************************************

Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muugano wa Tanzania imeishauri Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ( ICC) kukaa meza moja na nchi wanachama wa Mkataba wa Roma hususani zile za Afrika ili kutafuta suluhu ya changamoto na tofauti zilizopo kati ya mahakama hiyo na wanachama wake.
 
Tanzania imetoa wito huo siku ya jumatatu kupitia Mwakilishi wake wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lilipopokea na kujadili Taarifa ya Utendaji ya Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai.

Taarifa ICC imewasilishwa na Rais wa mahakama hiyo Jaji Slivia Fernandez de Gumendi katika kupindi ambacho Jumuiya ya Kimataifa imekumbwa na taharuki baada ya wanachama wawili wa Mkataba wa Roma, Afrika ya Kusini na Burundi kuwasilisha rasmi katika Umoja wa Mataifa kusudio la kujiondoa huku Gambia nayo ikitangaza kutaka kujitoa ingawa bado haijawasilisha rasmi nia yake hiyo.

Mwakilishi huyo wa Tanzania katika mchango wake amesema, uwepo au kuanzishwa kwa ICC kulitokana kwa kiasi kikubwa na uungwaji mkono kutoka Afrika. Akasema uungwaji mkono huo ulitokana hasa baada ya nchi hizo za Afrika kukatishwa tamaa na kuvunjika moyo baada ya kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

“Baada ya kukatishwa tamaa na kuvunjwa moyo, Mahakama hii, ilikuja kuwa chombo cha kutenda haki dhidi ya watu waliojihusisha na vitendo vya kikatili vikiwamo vya ukatili dhidi ya binadamu, uhalifu kivita na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Madhira yasiyoelezeka yaliyotokea Barani Afrika yakaifanya mahakama hii kuwa chombo cha matumaini dhidi ya wale ambao hawakuweza kuguswa au walikuwa juu ya sheria”. Akasema Balozi Manongi.