Thursday, November 3, 2016

Waziri Mahiga afungua Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na Usalama ya SADC


Waziri wa Mambo ya Nje na Uashirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC uliofanyika katika Ukumbi Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine katika Mkutano huo wanatarajia kujadilia hali ya kisiasa katika Nchi za Deokrasia ya Congo na Lesotho

Sehemu ya baadhi ya waandishi wa habari na wajumbe wa mkutano wakimsiliza Mhe. Waziri Dkt. Mahiga wakati akitoa hutuba ya ufunguzi.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) Dkt. Stregomena Tax akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda  Balozi Innocent Shiyo (kushoto) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC. Mezakuu  ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, (katikati) Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Aziz Mlima (kulia) na Katibu Mkuu SADC Dkt. Stregomena Tax (kushoto)

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.