Tuesday, November 1, 2016

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kutoka Liberia

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akizungumza na Mkurugenzi wa Mipango, Maendeleo na Uratibu kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Liberia, Bw. Theophilus Addey. Katika mazungumzo yao yalijikita katika kuelezea namna Serikali ya Tanzania inavyofanya kazi na Umoja wa Mataifa kupitia Mfumo wa One United Nations (One UN). Balozi Mushy alimweleza Bw. Addey kuwa Tanzania imekuwa nchi ya mfano wa kuigwa kutokana na mafanikio  makubwa yaliyofikiwa katika utekelezaji wa mfumo huo tangu kuanzishwa kwake hapa nchini mwaka 2007. Bw. Addey ameambatana na ujumbe wa pamoja kutoa Serikali ya Liberia na Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini humo.
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Bw. Addey wafuatilia mazungumzo.
Sehemu ya Maafisa wa Mambo ya Nje nao wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mushy na Bw. Addey (hawapo pichani)
Sehemu nyingine ya Maafisa Mambo ya Nje.
Balozi Celestine Mushy akimwelezea Bw. Theophilus Addey kitabu kinachoelezea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini
Balozi Mushy akiwa katia picha ya pamoja na ujumbe wa pamoja kati ya Serikali ya Liberia na Ofisi ya Umoja wa Mataifa. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.