Monday, November 28, 2016

Rais Lungu awasili Tanzania kwa ziara ya Siku tatu

Rais wa Jamhuri ya Zambia, Mhe. Edgar Lungu (kulia) akisalimiana na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam kwa ziara ya Kiserikali ya siku tatu.

Rais Lungu akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga huku Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia

Rais Lungu akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Aziz Mlima.

Rais Lungu akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Grace Mujuma

Rais Lungu akisalimiana na Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samuel Shelukindo

Rais Lungu na Mwenyeji wake Rais Magufuli wakiwa wamesimama wakati mizinga ya kumkaribisha Rais Lungu ikipigwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Rais Lungu akikagua gwaride lililoandaliwa kwa heshima yake

Viongozi mbalimbali wakiwemo Waheshimiwa Mabalozi wa nchi za Afrika wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakishuhudia mapokezi ya Rais Lungu

Rais Lungu na mwenyeji wake wakiangalia vikundi vya utamaduni vinavyotoa burdani uwanjani hapo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.