Thursday, November 3, 2016

WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA BALOZI WA UMOJA WA FALME ZA KIARABU NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Falme za kiarabu nchini Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Al Suweid katika mazungumzo yao balozi Al Suwied alimweleza Mhe. Waziri juu ya maandalizi ya Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) baina ya Tanzania na UAE ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 19 na 20, Dicemba, 2016 huko Abu Dhabi, UAE.
Wa kwanza kulia ni Katibu wa Waziri Bw. Gerald Mbwafu pamoja na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Hangson Mgaka, nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati Waziri Mahiga na Balozi Al Suweid (Hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea




********************************************


Tarehe 04 Novemba, 2016, Mhe. Dkt. Augustine P Mahiga (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Abdulla Ibrahim Ghanim Al Suweid, Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini. Balozi huyo alikuja kuzungumzia maandalizi ya Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) baina ya Tanzania na UAE ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 19 na 20, Disemba, 2016 huko Abu Dhabi, UAE. 

Sambamba na Mkutano wa JPC, Mheshimiwa Waziri na Balozi walizungumzia pia kuhusu ombi la UAE la kufanyika Kongamano la Biashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na UAE ambalo UAE imependekeza lifanyike wakati wa mkutano wa JPC huko Abu Dhabi, UAE.


Katika mkutano huo wa JPC maeneo ya ushirkiano ambayo yatazungumziwa na kukubaliwa ni pamoja na sekta ya Uchumi, Miundombinu (Bandari, Viwanja vya Ndege pamoja na Reli), Biashara, Uwekezaji, Viwanda, Kilimo, Afya, Utalii pamoja na Nishati ya Mafuta na Gesi. 

Aidha, viongozi hawa walizungumzia pia mikataba mbalimbali ambayo itasainiwa wakati wa mkutano huo wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano. Mheshimiwa Balozi alisisitiza kuwa Tanzania itumie fursa hii adhimu kwa kujiandaa kikamilifu katika kukuza ushirikiano wa kiuchumi na UAE. 

Kwa upande Mheshimiwa Waziri Mahiga alishukuru kupokea taarifa hiyo na kuahidi kufuatilia kwa karibu ili kuona Mkutano huo wa JPC unafanyika na kufanikiwa kwa manufaa za nchi zote mbili.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.