Friday, November 11, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Zambia nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi. Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi wa Zambia nchini, Mhe. Judith Kapijimpanga alimpomtembelea leo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao wamejadili masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili. Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa ni kuhusu kuboresha na kuimarisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inayoziunganisha Tanzania na Zambia, na masuala ya mazingira hasa kwa upande wa Ziwa  Tanganyika. 
Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akifafanua jambo kwa Balozi wa Zambia nchini Mhe.Kapijimpanga walipokutana kwa mazungumzo Wizarani
Mkutano ukiendelea
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Samuel Shelukindo (wa pili kulia) akifuatilia mazungumzo. Wa kwanza kulia  ni Afisa wa Wizara.
Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.