Thursday, November 3, 2016

Mkurugenzi wa ushirikiano wa Kimataifa akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy (kushoto) akifafanua jambo wakati akifanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa nchini Canada Mhe. Sarah Fountain Smith (kushoto) alipotembelea Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo wamezungumzia masuala mbalimbali ya kimaendeleo ya jamii na uchumi ambayo yanalenga kudumisha na kukuza uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akimsikiliza Naibu Waziri wa Canada Mhe.Sarah Fountain Smith wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Wizarani Jijini Dar es Salaam

Balozi Celestine Mushy akimkabidhi kitabu Mhe. Sarah Fountain Smith
Tokea kushoto; Balozi wa Canada nchini, Mhe.Ian Myles, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. Sarah Fountain Smith, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, maafisa kutoka Wizarani Bi. Ngusekela Nyerere na Bi. Lilian Kimaro  wakiwa katika picha ya pamoja.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.