Friday, November 4, 2016

Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Jeffrey Labovitz alipotembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji ametembelea nchini kwa mara ya kwanza toka shirika hilo lijiunge na Umoja wa Mataifa.  Mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili hali ya wakimbizi nchini, biashara haramu ya binadamu, hali ya wahamiaji haramu, na ushiriki wa watanzania wanaoishi ughaibuni katika kuchangia maendeleo ya nchi.
Waziri Mhe.Balozi Dkt. Mahiga akimsiliza Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Labovitz



Mkutano ukiendelea

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Mahiga na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Uhamaji Bw. Labovitz wakipeana mikono mara baada ya mazungumzo
Mkurugenzi wa Diaspora (Watanzania waishio ughaibuni) Balozi Anisa Mbega (kushoto) akiwa pamoja na maafisa wa Wizara wakifuatilia mazungumzo

Wakiwa katika picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.