Monday, November 28, 2016

Rais Magufuli ampokea Rais wa Zambia Ikulu, Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu alipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam. Mara baada ya mapokezi wawili hao waliketi kwa mazungumzo maalum yaliyokita katika kuendeleza miradi mbalimbali iliyoanzishwa na nchi hizo mbili ikiwemo reli (TAZARA) na bomba la mafuta (TAZAMA) ili iweze kuleta tija kwa wananchi.

Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu kabla ya kuanza mazungumzo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo  ya Nje na Ushirikino wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia, Mhe. Harry Kalaba wakisaini Mkataba wa utaratibu wa kushauriana kidplomasia kati ya Tanzania na Zambia.

Waziri wa Mambo  ya Nje na Ushirikino wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia, Mhe. Harry Kalaba wakipepongezana mara baada ya kutia saini mkataba.

Waziri wa Mambo  ya Nje na Ushirikino wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zambia, Mhe. Harry Kalaba wakionesha mkataba waliosaini kwa hadhira iliyokuwepo ukumbuni

Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edward Chagwa Lungu akizungumza na hadhira iliyokuwepo ukumbini mara baada ya kumaliza mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifuatilia mazungumzo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na hadhira waliokuwepo ukumbini mara baada ya kumaliza mazungumzo na Rais wa Zambia Mhe. Edgar Chagwa Rungu.

Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.