Wednesday, November 2, 2016

Balozi Msechu azindua zoezi la kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi

Balozi wa Tanzania katika Nchi za Nordic na Baltic mwenye makazi yake Sweden,  Mhe. Dora Msechu wa pili kutoka kulia akikata utepe kuashiria uzinduzi wa zoezi la kuchangia wahanga wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera lilifanyika Stockholm, Sweden. Hafla hiyo iliandaliwa na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Sweden kwa lengo la kuhamasisha Watanzania waishio Sweden kuchangia Wahanga wa Maafa ya tetemeko la ardhi Mkoani Kagera. Zoezi hili maalum la kuchangia maafa linaendelea mpaka tarehe 4 Novemba, 2016 na michango itakayopatikana itakabidhiwa kwa Mhe. Balozi Dora Msechu

Mhe. Balozi Dora Msechu akizungumza wakati wa hafla hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania katika Mji wa Malmo ambaye aliwasilisha salaam za watanzania waishio Malmo

Sehemu ya wadau walioshiriki hafla hiyo

Mwanadiaspora Mbarouk Rashidi akikabidhi vifaa kwa Mhe.Balozi Dora Msechu

Kocha Mkuu wa Kilimanjaro FC, Bw. Humphrey Kalanje akizungumza katika hafla hiyo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.