Thursday, March 23, 2017
Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho
Mhe. Sidibe Fatoumata KABA (katikati) akiwa ameongozana na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin (kushoto) na Mnikulu, Bw. Ngusa Samike. |
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha Balozi Kaba kwa Waziri Mahiga |
Mhe. Dmitry Kuptel akisikiliza wimbo wa taifa lake kutoka Bendi ya Polisi kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Magufuli |
Mhe. Dmitry Kuptel akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu |
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi Mokalake, Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu na Maafisa kutoka Ubalozi wa Botswana. |
Balozi ZAKAKARIAOU akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba |
Bendi ya Polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Mauritius kwa heshima ya Mhe. Balozi Jean Pierre Jhumun. |
Wednesday, March 22, 2017
Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ecuador nchini, Mhe. Benys Toscano Amores mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa New Zealand nchini, Mhe. Michael Gerrard Burrel mwenye makazi yake Pretoria, Afrika Kusini. |
Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi Mteule wa Oman nchini
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi (kushoto) akiwa na Bi. Patricia Kiswaga, Afisa Mambo ya Nje. |
Mazungumzo yakiendelea. |
Balozi Mlima akiagana na Balozi Al Mahruqi |
Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. |
Mazungumzo yakiendelea kushoto ni Maafisa wa Ubalozi wa Botswana ambao waliambatana na Mhe. Mokalake. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. |
Waziri Mahiga akiagana na Mhe. ZAKAKARIAOU mara baada ya kuwasilisha Nakala za Utambulisho. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Cyprus nchini, Mhe. Andreas Panayiotou mwenye makazi yake Muscat, Oman. |
Balozi Mero awasilisha Hati za Utambulisho
Balozi. Modest J. Mero akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. António Guterres. |
Balozi. Modest J. Mero na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. António Guterres wakipeana mikono baada ya zoezi la kuwasilisha Hati za Utambulisho kukamilika |
Akizungumza baada ya makabidhiano ya Hati za Utambulisho, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Guterres alisema Umoja wa Mataifa unaishukuru Tanzania kwa jinsi inavyojitolea kwa hali na mali katika jitihada za kumaliza migogoro ya kisiasa katika Ukanda wa Maziwa Makuu. Alitaja hatua zinazochukuliwa na Tanzania kurejesha amani DRC, Burundi na Sudan Kusini kuwa ni mfano wa kuigwa na kwamba anayo imani kwamba jitihada hizo hazitakoma mpaka nchi za SADC na EAC zote ziwe na utulivu wa kisiasa.Naye Balozi Mero akitoa neno la shukurani, alimuahidi Bw. Guterres ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na Umoja wa Mataifa katika kufanikisha malengo ya maendeleo na ulinzi wa amani. Aidha, alimwonyesha matarajio iliyonayo Tanzania kwake kwa kuzingatia ushirikiano mzuri aliounesha wakati alipokuwa akishughulikia masuala ya wakimbizi duniani, ambapo kwa pamoja na serikali ya Tanzania waliweza kutekeleza mengi kwa mafanikio makubwa
Tuesday, March 21, 2017
Timu ya Everton ya Uingereza kutua nchini hivi karibuni
Picha ya pamoja. |
Friday, March 17, 2017
Taarifa kuhusu Ziara ya Rais wa Benki ya Dunia nchini Tanzania
Taarifa
kuhusu Ziara ya Rais wa Benki ya Dunia nchini Tanzania
Rais wa Benki ya Dunia, Dkt. Jim Yong Kim, atafanya
ziara ya kikazi nchini kuanzia tarehe 19 hadi 21 Machi 2017. Akiwa nchini, Dkt.
Kim atafanya mazungumzo na Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Ikulu Jijini Dar Es Salaam siku ya Jumatatu, tarehe 20
Machi 2017 pamoja na kushiriki uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara
za Juu katika eneo la Ubungo (Ubungo Interchange).
Katika mazungumzo yao, Viongozi hao watajadili
namna bora ya kuimarisha zaidi uhusiano uliopo kati ya Tanzania na benki hiyo. Vilevile,
watazungumzia miradi mikubwa inayotarajiwa kutekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya
Dunia katika kipindi kijacho.
Aidha, baada ya mazungumzo hayo, Rais Magufuli na
mgeni wake watashuhudia uwekwaji saini wa mikataba mitatu: (i) Uboreshaji Miundombinu ya Usafiri Jijini
Dar es Salaam ikiwemo awamu ya tatu na ya nne ya mradi wa DART pamoja na ujenzi
wa barabara ya juu katika eneo la Ubungo (Dar es Salaam Urban Transport Project
(DUTP); (ii) Awamu ya pili ya mradi wa Uboreshaji
wa Upatikanaji wa Maji safi na uboreshaji wa miundombinu ya maji taka (Water
and Sanitation Project) na (iii) Uboreshaji wa Miundombinu na Huduma za msingi katika baadhi ya miji (Tanzania Strategic
Cities Project).
Wakati wa ziara hiyo, Dkt. Kim atapata pia fursa ya
kutembelea Shule ya Msingi Zanaki ambayo ni moja ya Shule zinazonufaika na
mpango wa kuboresha elimu ya msingi unaogharamiwa na Benki ya Dunia.
Ziara ya Dkt. Kim inafuatia ziara iliyofanywa
nchini na Makamu wa Rais wa Benki hiyo wa Kanda ya Afrika, Bw. Makhtar Diop mwezi
Januari 2017 ambapo alishiriki uzinduzi wa mradi wa mabasi ya mwendo kasi (BRT)
uliofanyika kwenye kituo kikuu cha mabasi hayo kilichopo Kariakoo jijini Dar Es
Salaam.
-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya
Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 17 Machi, 2017
Sunday, March 12, 2017
Waziri Mahiga ampokea Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani
Sehemu ya Wajumbe waliofuatana na Balozi Adt (hayupo pichani) nao wakifuatilia mazungumzo |
Mazungumzo yakiendelea |
Waziri Mahiga akiagana na Balozi Adt mara baada ya kumaliza mazungumzo. |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Taarifa kuhusu Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amesema kuwa Tanzania na Ujerumani zitaendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo yale yanayohusu kudumisha amani na usalama duniani pamoja na kuheshimu misingi ya haki za binadamu kupitia Jumuiya za Kikanda na Kimataifa.
Mhe. Waziri Mahiga ameyesema hayo alipokutana kwa mazungumzo na Balozi Harro Adt, Mjumbe Maalum wa Kansela wa Ujerumani, Mhe. Angela Merkel kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli alipofika Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe huo.
Katika mazungumzo yao, Mhe. Waziri Mahiga alisema kuwa, Ujerumani na Tanzania zina mahusiano ya kihistoria tangu enzi za ukoloni hadi sasa. Katika masuala ambayo Tanzania inanufaika na ushirikiano huo ni pamoja na ujenzi wa miundombinu, maboresho katika sekta ya elimu na mchango katika uhifadhi wa wanayamapori.
“Uhusiano wa Tanzania na Ujerumani ni wa kihistoria tangu ukoloni. Hata hivyo Ujerumani wamejaribu kutafsiri ushirikiano wetu katika misingi bora sasa kuliko ile ya kikoloni. Ujerumani imekuwa ikiisaidia Tanzania moja kwa moja katika sekta mbalimbali kama elimu, wanyamapori na miundombinu na misaada mingine imekuwa ikipitia Umoja wa Ulaya” alisema Waziri Mahiga.
Akizungumzia ziara ya Balozi Adt nchini, Mhe. Waziri Mahiga alisema Mjumbe huyo Maalum wa Kansela wa Ujerumani ameleta ombi kwa Mhe. Rais na kwa Watanzania la kuiunga mkono Ujerumani kwenye nafasi ya Mjumbe asiye wa Kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wa uchaguzi utakaofanyika mwaka 2018. Aliongeza kusema kuwa, Ujerumani imedhamiria kugombea nafasi hiyo ikiwa na dhamira ya kuunga mkono mageuzi ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ikiwemo kuziunga mkono nchi za Afrika kwenye harakati za kupatiwa nafasi mbili za kudumu kwenye Baraza hilo.
Aidha, Mhe. Waziri Mahiga alifafanua kwamba, katika kufikia malengo hayo Ujerumani imejiwekea misingi mikuu minne ambayo ni:- Kusaidia jitihada za amani na usalama duniani; Kusimamia Haki ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa; Kuhamasisha mageuzi ya Teknolojia na Kuhimiza ushirikiano na Ubia wa Kimataifa.
Mhe. Mahiga alieleza kuwa kwa kuzingatia misingi hiyo, amemueleza Balozi Adt azma ya Tanzania kuiomba Ujerumani iisadie Afrika kujenga Jengo la Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ambapo Tanzania ndio Makao yake Makuu huko Mjini Arusha.
Mhe. Mahiga pia alimhakikishia Balozi Adt kuwa ameupokea ujumbe wa Kansela wa Ujerumani na atauwasilisha kwa Mhe. Rais.
Kwa upande wake Balozi Adt, Mjumbe Maalum kutoka Ujerumani alisema kuwa amefurahishwa na mapokezi aliyoyapata baada ya kuwasili nchini. Pia ana imani kuwa Tanzania ambao ni rafiki wa kihistoria wa Ujerumani itawaunga mkono kwenye nafasi hiyo ili kuwawezesha kutekeleza malengo waliyojiwekea ikiwemo kuhakikisha Afrika inapata nafasi mbili za kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 12 Machi, 2017
Subscribe to:
Posts (Atom)