Wednesday, March 22, 2017

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi Mteule wa Oman nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (kulia) akizungumza na Balozi Mteule wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Mahruqi alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika suala la Makao Makuu ya Serikali kuhamia Dodoma na namna Ofisi za Ubalozi huo zinavyoweza kutumia fursa hiyo kuwashauri wafanyabiashara wa Oman kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu pamoja na huduma nyingine za biashara ambazo bado hazijawa za uhakika katika mji huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi (kushoto) akiwa na Bi. Patricia Kiswaga, Afisa Mambo ya Nje.
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi Mlima akiagana na Balozi Al Mahruqi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.