Thursday, March 23, 2017

Mhe. Rais Magufuli apokea Hati za Utambulisho

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Hungary nchini, Mhe. Laszlo Eduard Mathe mwenye makazi yake Nairobi, Kenya. Hafla hiyo fupi imefanyika tarehe 23 Machi, 2017, Ikulu, Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Mathe akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa kwanza kulia), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mary Matari wakishuhudia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Guinea nchini, Mhe. Sidibe Fatoumata KABA mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. Hafla hiyo fupi imefanyika tarehe 23 Machi, 2017, Ikulu, Dar es Salaam.
Mhe. Sidibe Fatoumata KABA (katikati) akiwa ameongozana na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin (kushoto) na Mnikulu, Bw. Ngusa Samike.
Mhe. Rais Magufuli akimtambulisha Balozi Kaba kwa Waziri Mahiga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. Hafla hiyo fupi imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017.
Mhe. Dmitry Kuptel akisikiliza wimbo wa taifa lake kutoka Bendi ya Polisi kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Magufuli
Mhe. Dmitry Kuptel akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Botswana nchini, Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake mwenye makazi yake Lusaka, Zambia. Hafla hiyo fupi imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 23 Machi, 2017
Balozi Mokalake akisikiliza wimbo wa taifa lake kutoka Bendi ya Polisi kabla ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin na kushoto ni Mnikulu, Bw. Ngusa Samike
Mhe. Rais Magufuli akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi Mokalake, Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu na Maafisa kutoka Ubalozi wa Botswana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho  kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia.
Balozi ZAKAKARIAOU akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea Hati za Utambulisho  kutoka kwa Balozi  wa Mauritius nchini, Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake Maputo, Msumbiji.
Bendi ya Polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Mauritius kwa heshima ya Mhe. Balozi Jean Pierre Jhumun.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.