Thursday, March 30, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje apokea Nakala za Utambulisho za Mabalozi Wateule kutoka Ethiopia na Vietnam nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Vietnam nchini,  Mhe. Nguyen Kim Doanh. Tukio hilo limefanyika Wizarani tarehe 30 Machi, 2017.
Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Vietnam, Mhe. Nguyen Kim Doanh mara baada ya  kupokea nakala zake za hati za utambulisho
Balozi Mteule Mhe. Nguyen Kim Doanh naye akizungumza.
Dkt. Kolimba na Balozi Mteule Mhe. Nguyen Kim Doanh wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Magabilo Murobi na Afisa kutoka Ubalozi wa Vietnam nchini
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini, Mhe. Dina Mufti Sid.Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 30 Machi, 2017.
Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Ethiopia nchini, Mhe. Dina Mufti Sid.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.