Tuesday, March 21, 2017

Timu ya Everton ya Uingereza kutua nchini hivi karibuni

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Bw. Luca Neghesti kutoka SportPesa Tanzania leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Bw. Neghesti amefuatana na wawakilishi wa timu ya Mpira wa Miguu ya Everton ya nchini Uingereza kumpa taarifa Mhe. Waziri kuhusu maandalizi ya kuileta timu hiyo kucheza mechi za kirafiki nchini Tanzania hivi karibuni.


Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na wawakilishi wa timu ya mpira ya Everton ya nchini Uingereza. Timu hiyo ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuja Tanzania kwa ajili ya kucheza mechi za kirafiki. Mhe. Waziri alisema ziara hiyo itasaidia kuitangaza Tanzania duniani pamoja na kuhamasisha mchezo wa mpira wa miguu kwa vijana wa Kitanzania. Anaozungumza nao kutoka kulia ni Mkuu wa Uendeshaji wa Mpira wa Miguu (Head of Football Operations) wa timu hiyo, Bw. David Harrison; Mkuu wa Ulinzi na Usalama (Head of Safety and Security) wa timu, Bw. Dave Lewis na Bw. Alan Chisholm kutoka Thomas Cook.


Waziri Mahiga akifurahia zawadi ya jezi aliyokabidhiwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Mpira wa Miguu (Head of Football Operations) wa timu ya Everton, Bw. David Harrison. Jezi hiyo ni ya Mchezaji wa Timu hiyo ambaye pia ni Nahodha wa Timu ya Taifa ya Ireland, Bw. Coleman.

Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.