Thursday, March 2, 2017

Kamati ya Kusimamia Soko la Pamoja la EAC yakutana jijini Dar Es Salaam

Mkurugenzi wa Ajira kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Bw. Amir Amir aliyeshika kipaza sauti ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao cha Kamati ya kusimamia utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki akifungua kikao hicho jana kwenye ukumbi wa hoteli ya Holiday In jijini Dar Es Salaam.

Bi. Agatha Nderitu akiwasilisha matokeo ya utafiti wa namna nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zilivyotekeleza Itifaki ya Soko la Pamoja kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2014 hadi 2016. Utafiti huo ulilenga maeneo ya Soko huru la bidhaa, mitaji na uhuru wa watu kusafiri ndani ya Jumuiya. Utafiti huo ulionesha kuwa nchi za EAC zimejitahidi kutekeleza Itifaki hiyo ingawa bado kuna vikwazo na sheria zinazozuia utekelezaji wa soko hilo kikamilifu hususan kwenye vikwazo visivyo vya kibiashara.

Baadhi ya washiriki wakifuatiliwa mada kuhusu tathmini ya utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.