Friday, March 31, 2017

Waziri Mkuu wa Ethiopia awasili nchini kuanza ziara ya siku mbili

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (kushoto) akimpokea Waziri Mkuu wa Shirikisho la Kidemokrasia ya Jamhuri ya Ethiopia nchini Mhe. Hailemariam Dessalegn mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mhe. Dessalegn yupo nchini kwa ziara ya siku mbili ambapo atafanya mazungumzo yake na Rais Magufuli pamoja na kutembelea Bandarini.   
Rais Magufuli pamoja na Mhe. Dessalegn wakiwa kwenye jukwaa tayari kwa kupigiwa nyimbo za taifa.
Waziri Dessalgn akikagua gwaride maalumu lililoandaliwa wakati wa mapokezi yake
Waziri Mkuu Dessalegn akiwapungia mkono wananchi waliojitokeza kumpokea mara baada ya kuwasili.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.