Wednesday, March 1, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa DPRK nchini

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea (DPRK) nchini, Mhe. Kim Yong Su, alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na kuzungumzia historia ya ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Tanzinia na DPRK pia walizungumzia ushirikiano katika masuala ya uchumi, hususan katika ujenzi wa miundombinu na kilimo chenye tija.
Mhe. Balozi Kim Yong Su nae akimweleza jambo Mhe. Dkt. Susan ambapo alitumia fursa hiyo kueleza namna Serikali DPRK ilivyojidhatiti katika kuhakikisha ushirikiano unazidi kuimarika kwa faida ya mataifa hayo mawili.
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo.Kushoto ni Bw. Benedict Msuya na pembeni yake ni Bw. Charles Faini.

Mazungumzo yakiendelea.
Picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.